“KARIAKOO DERBY” SIMBA YAJICHIMBIA ZANZIBAR, YANGA IKISALIA DAR.

 

JOTO la kuelekea mchezo wa watani wa jadi kati ya Yanga na Simba likiendelea kupanda timu ya wekundu wa msimbazi Simba wameamua kusafiri hadi visiwani Zanzibar kwa kambi ya maandalizi kuelekea mchezo huo huku Yanga ikisalia Jijini Dar es salaam kujifua kwenye uwanja wa Avic Town Kigamboni.

Simba ina kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo uliopita walipokubali kichapo cha mabao 5-1 mbele ya Yanga katika uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es salaam.

Mchezo huo wa Watani wa Jadi utapigwa Aprili 20, kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia saa 11:00 jioni.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *