FIRST LEAGUE NANE BORA KUANZA KUTIMUA VUMBI LEO.

 

MICHUANO ya First League hatua ya Nane Bora inaanza kutimua vumbi leo Mei 2 mkoani Tanga ikishirikisha jumla ya timu nane kutoka mikoa tofauti.

Mchezo wa ufunguzi utazikutanisha African Sports ya Tanga dhidi ya Malimao ya Dar es salaam saa 8:00 mchana katika uwanja wa CCM Mkwakwani ikifuatiwa na mchezo wa saa 10:00 alasiri kati ya Rhino Rangers na Nyumbu.

Timu shiriki ni Nyumbu ya Pwani, African Sports ya Tanga, Kiluvya na Malimao za Dar, Mapinduzi ya Mwanza, Rhino Rangers ya Tabora, Tanesco ya Kilimanjaro na Mwadui ya Shinyanga ambazo zimegawanya kwenye makundi mawili, ya A na B.

Timu mbili za juu kutoka kila kundi zitafuzu moja kwa moja hatua ya nusu fainali huku timu zitakazoingia fainali zitakata tiketi ya kushiriki Ligi ya NBC Championship msimu ujao wa 2024/2025.

Timu mbili zitakazopoteza hatua ya Nusu fainali zinayo nafasi ya kupanda Ligi ya NBC Championship kwa kucheza michezo ya mchujo na timu zilizopoteza mchezo wa mchujo wa Kubaki Ligi ya NBC Championship na mshindi wa jumla kushiriki Ligi ya NBC Championship msimu ujao wa 2024/2025.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *