MCHEZO wa Ligi Kuu ya NBC ‘Derby’ ya Mzizima unapigwa leo kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa saa 12:15 jioni kati ya Azam na Simba.
Mchezo huu unabeba hisia za watu wengi kutokana na nafasi za kila timu kwenye msimamo huku ukiwa ni mchezo wa hatma za timu hizi kwenye nafasi ya kuendelea kupambania ubingwa.
Mchezo wa Mzunguko wa kwanza Simba dhidi ya Azam ulimalizika kwa Sare ya bao 1, bao la Azam likifungwa na Prince Dube huku lile la Simba likifungwa na Clatous Chama.
Kwenye msimamo Azam ipo nafasi ya Pili ikiwa na alama 57 baada ya michezo 25 huku Simba ikiwa nafasi ya Tatu ikiwa na alama 53 kwenye michezo 24 pungufu ya mchezo mmoja nyuma ya Azam.