COASTAL KUJIULIZA KWA MASHUJAA LEO KWENYE LIGI KUU YA NBC.

BAADA ya Singida Black Stars na Dodoma Jiji kutamba kwenye uwanja wa nyumbani jana kwa ushindi jana timu ya Coastal Union leo itakuwa mwenyeji wa Mashujaa kuzisaka alama tatu muhimu.

Coastal iliyochagua kutumia uwanja wa KMC uliopo Dar kama uwanja wa nyumbani kwenye mchezo huu itacheza huku ikipambana kupata ushindi wa kwanza msimu huu dhidi ya Mashujaa ambayo haijapoteza mchezo wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu.

Coastal ilipata sare ya bao moja kwenye mchezo wake uliopita dhidi ya KMC baada ya Maabad Maabad kusawazisha dakika za mwisho kwa mkwaju wa penati.

Mashujaa ni miongoni mwa timu saba za Ligi Kuu ya NBC ambazo bado hazijaruhusu bao lolote msimu huu ikiungana na timu za Simba, Yanga, Pamba Jiji, Azam, Tanzania Prisons na JKT Tanzania.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *