‘KIVUMBI’ CHA LIGI KUU YA NBC KUENDELEA.

BAADA ya Tabora United na Fountain Gate kupata ushindi hapo jana Ligi Kuu ya NBC inaendelea tena leo kwa michezo miwili itakayopigwa mikoa miwili tofauti.

Saa 10:00 alasiri timu ya Singida BS ya Singida itakuwa mwenyeji wa KMC ya Dar kwenye uwanja wa Liti, Singida.

Singida imeshinda michezo yote miwili ya kwanza msimu huu iliyocheza ugenini na leo itaikaribisha KMC kwenye mchezo wa kwanza katika uwanja wa nyumbani.

Mchezo wa pili utachezwa saa 10:00 alasiri kama mchezo wa awali kati ya timu ya Dodoma Jiji na Namungo ya Lindi kwenye uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara.

Timu zote mbili hazijapata ushindi kwenye mchezo wowote wa Ligi Kuu ya NBC hadi sasa na hivyo kufanya mchezo huu kuwa na ushindani mkubwa.

2 comments

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *