AHOUA ‘HACHEKI NA WOWOTE’ LIGI KUU NBC.

JEAN Ahoua wa timu ya Simba ameendelea kuwa na msimu bora wa Ligi Kuu ya NBC hadi sasa baada ya kuhusika kwenye mabao 19 huku timu yake ikisalia na michezo nane kutamatisha msimu.

Ahoua aliyesajiliwa na Simba akitokea Asec Mimosa mpaka sasa amehusika katika mabao 19  baada ya kufanikiwa  kufunga mabao 12 kutoa pasi zilizozaa mabao saba hivyo kufanya kuwa mchezaji aliyehusika katika mabao mengi kuliko mchezaji yeyote.

Prince Dube  ambaye amesajiliwa  na timu ya Young Africans akitokea Azam  anashikilia nafasi ya pili akiwa amehusika katika mabao 17 baada ya kufunga mabao 10 na kutoa pasi za mabao saba.

Mpinzani wa karibu wa Dube ni Feisal Salum wa Azam akiwa amefanikiwa kutoa pasi za mwisho 12 na kufunga mabao manne  hivyo kuhusika katika mabao 16.

Kwa upande wake Aziz Ki wa Young Africans amefanikiwa kufunga mabao saba na kutoa pasi za mabao saba hivyo kuhusika katika mabao 14.

Pacome Zouzoua na Clement Mzize wa Young Africans wote wamehusika katika mabao 13 kila mmoja  huku Pacome akifunga mabao saba na kutoa pasi za mwisho sita huku Mzize akifunga mabao 10 na kutoa pasi za mwisho tatu.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *