MWALIMU KINARA WA TUZO LIGI YA NBC.

Mchezaji wa Fountain Gate Seleman Mwalimu ameendelea kuwa mwiba kwa mabeki wa timu za Ligi Kuu ya NBC kutokana na kufunga mabao sita hivyo kuwa mshambuliaji hatari zaidi awapo langoni mwa mpinzani.

Licha ya kuongoza kwa idadi kubwa ya mabao pia Mwalimu anaongoza kuwa na tuzo nyingi kuliko mchezaji yoyote wa Ligi hiyo baada ya kufikisha tuzo tano.

Mwalimu amefanikiwa kuwa mchezaji bora wa michezo minne tofauti ya Fountain Gate dhidi ya KMC, Tanzania Prisons, Dodoma Jiji na KenGold.

Aidha Mwalimu alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi septemba hivyo kumfanya kuwa mchezaji mwenye tuzo tano katika Ligi Kuu ya NBC.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *