TIMU ya Mashujaa imeshindwa kubaki na alama zote tatu nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya bao moja na timu ya KMC kwenye uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma.
Mchezo ulianza kwa kila timu kupambania timu yake na dakika ya 11 Mundhur Vuai wa Mashujaa aliifungia timu yake bao la kuongoza na kuwanyanyua mashabiki wa Mashujaa waliojitokeza uwanjani.
Ikisalia dakika moja mchezo kumalizika huku Mashujaa ikiamini imeshakusanya alama zote tatu mchezaji Akramu Muhina aliisawazishia KMC na kufanya timu hizo kugawana alama.
Mashujaa imesalia nafasi ya 7 na alama 34 huku KMC ikiwa na alama 34 kwenye nafasi ya 10 na kujihakikishia nafasi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26.Akram Muhina wa KMC ndiye aliibuka mchezaji bora wa mchezo baada ya kuiokoa timu yake kwa bao la ugenini na kuipa tiketi ya Ligi Kuu ya NBC msimu ujao.