KAGERA SUGAR RASMI NBC CHAMPIONSHIP

 

 

TIMU ya Kagera Sugar imeaga rasmi Ligi Kuu ya NBC baada ya timu ya Pamba Jiji kuifunga KenGold 0-2 ugenini na kufikisha alama 30 ambazo haziwezi kufikiwa na Kagera ikiwa itashinda michezo yake miwili iliyosalia.

Pamba Jiji ilipata bao lake la kuongoza kipindi cha kwanza lililofungwa na mchezaji Yonta Camara dakika ya 30 anayecheza kwa mkopo kwenye timu hiyo kutokea Singida Black Stars.

Kipindi cha pili Yonta Camara kwa mara nyingine aliipatia bao la pili timu yake Dakika ya 60 na kufanya matokeo kuwa 0-2 hivyo kuzamisha matumaini ya Kagera kuendelea kusalia Ligi Kuu ya NBC .

Pamba jiji imefikisha alama 30 ikiwa nafasi ya 11 huku KenGold ikiwa tayari imeshuka daraja baada ya kukusanya alama 16 ikicheza msimu mmoja pekee wa Ligi Kuu ya NBC tangu kupanda ligi ya NBC championship.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *