TIMU ya Young Africans ‘Wananchi’ imezidi kuchanja mbuga kwenye mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kushinda mchezo wa 11 Kwenye michezo 13 ikiwa haijapoteza hata mmoja na kutoa sare miwili pekee.
’Wananchi’ wameongeza ushindi huo baada ya kuifunga Tanzania Prisons iliyokuwa mwenyeji wa mchezo huo uliopigwa uwanja wa Jamhuri, Dodoma baada ya uwanja wao ‘mama’ wa Sokoine, Mbeya kufungiwa kupisha maboresho.
Laurindo Dilson ‘Depu’ aliandika bao lake la sita msimu huu likiwa bao pekee lililopeleka furaha kwenye mitaa ya ‘Jangwani’ baada ya mchezo uliopita Young Africans kutoa sare na mahasimu wao wakubwa timu ya Simba.
Young Africans wanaendelea kujichimbia kwenye ‘kilele’ cha Ligi Kuu ya NBC wakifikisha jumla ya alama 35 baada ya kucheza michezo 13 huku timu inayowafuata kwa karibu (JKT Tanzania) ikicheza michezo … zaidi ya ‘Wananchi’.
Ingawa Depu aliingia kwenye mchezo huo alifanikiwa kuondoka na tuzo ya mchezaji bora wa mchezo hii ni baada ya bao alilofunga na kiwango alichokionyesha kuipa alama tatu muhimu Young Africans ambao ndio mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya NBC.