TIMU ya Singida imepata ushindi wa pili msimu huu baada ya kuifunga Namungo mabao 2-3 kwenye uwanja wa Majaliwa, Lindi.
Namungo haijashinda mchezo wowote wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu ikipata sare mitatu na kupoteza mitatu.
Singida imeshinda michezo miwili idadi sawa na michezo ya kufungwa na kupata sare.
Mabao mawili yaliyofungwa na Marouf Tchakei na moja la Duke Abuya yameifanya Singida kufikisha alama nane na kukwea mpaka nafasi ya sita kwenye msimamo.