Author: Loveness Bernard

SIMBA, PRISONS ZANG’ARA LIGI KUU YA NBC.

TIMU za Simba na Tanzania Prisons zimetakata katika viwanja vya nyumbani baada ya kuibuka na ushindi katika michezo yao ya kukamilisha mzunguko wa 26.

Mchezo Simba na Pamba ulianza kwa kasi kila timu ikicheza kwa tahadhari kubwa ambapo ilimchukua dakika saba kiungo wa Simba, Ellie Mpanzu kufungua ukurasa wa mabao na dakika ya 18 Mathew Tegisi wa Pamba alisawazisha hivyo mchezo kwenda mapumziko wakiwa sare ya 1-1.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu kushambuliana na dakika ya 64 mchezaji wa Simba Libase Gueye aliipatia Simba bao la pili hivyo mpaka mchezo unatamatika Simba ilipata ushindi wa 2-1.

Kwa upande wa mchezo uliopigwa Sokoine timu ya Tanzania Prisons iliikaribisha Dodoma Jiji kwenye mchezo ulikuwa wa kushambuliana na dakika mbili zilimtosha Fransisco Lulihoshi kufungua akaunti ya magoli kupitia mkwaju wa penati .

Oscar Mwajanga aliiongezea bao la pili Prisons dakika ya 12 huku Waziri Junior wa Dodoma akifunga bao la kufutia machozi kwa timu yake dakika ya 43 hivyo kwenda mapumziko 2-1.

Kipindi cha pili kilirejeahuku Dodoma ikionekana kushambulia zaidina hata hivyo Oscar Mwajanga alizidi kudidimiza matumaini yao baada ya kufunga bao la 3 hivyo mchezo kuisha 3-1.

MBILI ZA MOTO LEO LIGI KUU YA NBC.

MZUNGUKO wa 26 wa Ligi Kuu ya NBC unatamatika leo kwa michezo miwili itakayochezwa mkoani Dar es Salaam na Mbeya.

Wachezaji wa Simba.

Simba iliyopo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC inayosaka nafasi ya kutwaa ubingwa itakuwa mwenyeji wa timu ya Pamba Jiji kutoka jijini Mwanza inayoshika nafasi ya saba ambapo timu hiyo inatafuta kujiimarisha katika nafasi nzuri huku mchezo huo ukitarajiwa kupigwa kwenye uwanja wa KMC Complex majira ya saa kumi jioni.

Wachezaji wa Pamba Jiji

Sambamba na mchezo huo Tanzania Prisons iliyopo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikisaka kujinasua kushuka daraja itaikaribisha timu ya Dodoma Jiji inayoshika nafasi ya nane kwenye msimamo wa Ligi hiyo ambayo pia inatafuta kujiweka katika nafasi nzuri.

NBC CHAMPIONSHIP YA MOTO LEO.

MZUNGUKO wa 29 wa Ligi ya NBC Championship unaendelea leo kwa michezo nane itakayochezwa majira ya saa kumi jioni.

Mchezo wa kwanza utakuwa uwanja wa Majimaji ambapo Songea United itakuwa mwenyeji wa timu ya Hausung huku Ken Gold ikichuana na B19 kwenye uwanja wa Chunya mkoani Mbeya.

Polisi Tanzania itaikaribisha timu ya Mbeya Kwanza katika uwanja wa Usharika mkoani Kilimanjaro mchezo utakaokuwa mbashara kwenye chaneli ya FIFA +, huku African Sports ikimenyana na Bigman kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Kagera Sugar itachuana na Gunners katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera huku Stand United ikicheza na Geita Gold katika uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga.

TMA na Barberian zitacheza katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha huku Transit Camp ikichuana na Mbuni kwenye uwanja wa TFF Kigamboni.

AZAM YATAKATA ARUSHA, KMC IKISHUKA DARAJA.

TIMU ya Azam imetakata katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kuvuna alama tatu na mabao mawili baada ya kuichapa timu ya Fountain Gate katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid .

Mchezo huo uliopigwa saa kumi jioni ulianza kwa timu zote kushambuliana kwani kila timu ilizitaka alama tatu muhimu.

Ilimchukua dakika 36 mshambuliaji wa Azam Jean Ngita kufungua ukurasa wa mabao ambapo timu hiyo ilienda mapumziko ikiwa mbele kwa 0-1.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi Fountain wakitaka kusawazisha ambapo dakika ya 64 mshambuliaji wa Azam Jephte Kitambala aliongeza bao la pili kwa timu yake na hadi mchezo huo unatamatika matokeo ni 0-2.

Mkwakwani Tanga wenyeji Coastal Union waliikaribisha Namungo
ambapo timu zote zilihitaji alama ili kujiweka katika nafasi nzuri na dakika 37 ziliwatosha Coastal kupata bao la kuongoza kupitia mchezaji Robert Savilla kabla ya timu ya Namungo kusawazisha kipindi cha pili dakika ya 62 kupitia mchezaji Geofrey Luzindaze hivyo mchezo kumalizika kwa sare ya 1-1.

Saa mbili usiku KMC ilikuwa na kibarua kizito cha kuikaribisha timu ya TRA katika uwanja wa KMC Complex mchezo ulioanza kwa KMC kuonekana ikizitaka alama tatu muhimu hata hivyo haikuweza kufanikiwa baada ya kukubali kipigo cha 0-1z

Ilimchuka dakika 12 beki wa TRA Chamou Karaboue kuipatia bao timu yake ambalo limebaki kuwa bao pekee kufungwa katika mchezo huo mpaka dakika 90 zilipotamatika na hivyo timu ya KMC kushuka daraja kwani hata ikishinda michezo yake iliyosalia haitaweza kutoka kwenye mstari wa kushuka daraja.

GREEN WARRIORS YAAGA RASMI FIRST LEAGUE.

TIMU ya Green Warriors imeshuka daraja rasmi baada ya kupoteza mchezo wa leo kwa 3-2 dhidi ya Nyumbu ugenini kwenye mchezo wa Ligi ya First League.

Green imekusanya alama 11 kwenye michezo 14 iliyocheza ambazo hazikutosha kuwaweka salama kwenye ligi hiyo na hivyo kushuka hadi Ligi ya Mabingwa wa Mikoa kwa msimu wa 2026/27.

Nyumbu yenye alama 29 ilicheza michezo 14 ushindi nane, sare tano na kupoteza mchezo mmoja imeshika nafasi ya pili hivyo kukata tiketi ya kucheza hatua ya mtoano.

Cosmopolitan iliyopo nafasi ya tatu nayo itacheza hatua ya mtoano baada ya kufikisha alama 22 kwa kucheza michezo 14, ushindi michezo saba,sare moja na kufungwa michezo sita.

Moro Kids na timu ya Dar City zimesalia kucheza First League 2026/2027 baada ya kushika nafasi ya nne na tano kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Kwa upande wa Magnet na Pan African zitacheza michezo ya mchujo wa First League na timu zilizoshika nafasi ya sita na saba kutoka Kundi B.