Author: Loveness Bernard

AZAM YATAKATA ARUSHA, KMC IKISHUKA DARAJA.

TIMU ya Azam imetakata katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kuvuna alama tatu na mabao mawili baada ya kuichapa timu ya Fountain Gate katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid .

Mchezo huo uliopigwa saa kumi jioni ulianza kwa timu zote kushambuliana kwani kila timu ilizitaka alama tatu muhimu.

Ilimchukua dakika 36 mshambuliaji wa Azam Jean Ngita kufungua ukurasa wa mabao ambapo timu hiyo ilienda mapumziko ikiwa mbele kwa 0-1.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi Fountain wakitaka kusawazisha ambapo dakika ya 64 mshambuliaji wa Azam Jephte Kitambala aliongeza bao la pili kwa timu yake na hadi mchezo huo unatamatika matokeo ni 0-2.

Mkwakwani Tanga wenyeji Coastal Union waliikaribisha Namungo
ambapo timu zote zilihitaji alama ili kujiweka katika nafasi nzuri na dakika 37 ziliwatosha Coastal kupata bao la kuongoza kupitia mchezaji Robert Savilla kabla ya timu ya Namungo kusawazisha kipindi cha pili dakika ya 62 kupitia mchezaji Geofrey Luzindaze hivyo mchezo kumalizika kwa sare ya 1-1.

Saa mbili usiku KMC ilikuwa na kibarua kizito cha kuikaribisha timu ya TRA katika uwanja wa KMC Complex mchezo ulioanza kwa KMC kuonekana ikizitaka alama tatu muhimu hata hivyo haikuweza kufanikiwa baada ya kukubali kipigo cha 0-1z

Ilimchuka dakika 12 beki wa TRA Chamou Karaboue kuipatia bao timu yake ambalo limebaki kuwa bao pekee kufungwa katika mchezo huo mpaka dakika 90 zilipotamatika na hivyo timu ya KMC kushuka daraja kwani hata ikishinda michezo yake iliyosalia haitaweza kutoka kwenye mstari wa kushuka daraja.

GREEN WARRIORS YAAGA RASMI FIRST LEAGUE.

TIMU ya Green Warriors imeshuka daraja rasmi baada ya kupoteza mchezo wa leo kwa 3-2 dhidi ya Nyumbu ugenini kwenye mchezo wa Ligi ya First League.

Green imekusanya alama 11 kwenye michezo 14 iliyocheza ambazo hazikutosha kuwaweka salama kwenye ligi hiyo na hivyo kushuka hadi Ligi ya Mabingwa wa Mikoa kwa msimu wa 2026/27.

Nyumbu yenye alama 29 ilicheza michezo 14 ushindi nane, sare tano na kupoteza mchezo mmoja imeshika nafasi ya pili hivyo kukata tiketi ya kucheza hatua ya mtoano.

Cosmopolitan iliyopo nafasi ya tatu nayo itacheza hatua ya mtoano baada ya kufikisha alama 22 kwa kucheza michezo 14, ushindi michezo saba,sare moja na kufungwa michezo sita.

Moro Kids na timu ya Dar City zimesalia kucheza First League 2026/2027 baada ya kushika nafasi ya nne na tano kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Kwa upande wa Magnet na Pan African zitacheza michezo ya mchujo wa First League na timu zilizoshika nafasi ya sita na saba kutoka Kundi B.

LIGI KUU YA NBC YAREJEA.

LIGI Kuu ya NBC inarejea leo kwa michezo mitatu itakayochezwa Dar es Salaam, Arusha na Tanga baada ya mapumziko ya takribani wiki mbili kupisha michezo ya kalenda ya FIFA.

Michezo miwili ya kwanza itapigwa majira ya saa kumi jioni mkoani Arusha kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid ambapo timu ya Fountain Gate iliyopo nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Lgi Kuu ya NBC itaikaribisha timu ya Azam iliyopo nafasi ya tatu kwenye msimamo.

Mchezo mwingine utakaopigwa muda huo ni kati ya Coastal Union iliyopo nafasi ya 10 kwenye msimamo wa Lgi Kuu ya NBC itakuwa mwenyeji wa timu ya Namungo iliyopo nafasi ya 13 katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Mchezo wa mwisho utakuwa jijini Dar es Salaam ambapo KMC iliyopo nafasi ya 16 kwenye msimamo wa Lgi Kuu ya NBC itaikaribisha timu ya TRA katika uwanja wa KMC Complex majira ya saa mbili usiku ukiwa ni mchezo wa mwisho wa kukamilisha siku.

OKELLO, BARKER WANG’ARA TUZO MEI.

KIUNGO mshambuliaji  wa Young Africans, Allan Okello, amechaguliwa kuwa mchezaji Bora wa mwezi Mei wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2025/26, huku Steve Barker wa Simba  akichaguliwa Kocha Bora wa ligi hiyo kwa mwezi huo.

Mchezaji wa Young Africans, Allan Okello.

Okello alionyesha kiwango kizuri chenye mwendelezo kwa mwezi huo ikiwa ni pamoja na kufunga mabao tisa na kuhusika na lingine moja kwa kutoa pasi ya usaidizi  katika dakika 509 za michezo sita, ambayo Young Africans ilicheza nakuisaidia kubaki kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Mchezaji huyo aliwashinda viungo Clatous Chama wa Simba na Feisal Salum wa Azam alioingia nao fainali katika mchakato wa Tuzo za Mwezi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker.

Kwa upande wa Barker aliyeingia fainali na Florent Ibenge wa Azam na Fred Minziro wa Fountain Gate, aliiongoza timu yake kushinda michezo mitanoi liyocheza na kutoka sare mmoja na kuendelea kubaki nafasi ya pili kwenyemsimamo wa ligi.

Wakati huohuo Meneja wa Uwanja wa Airtel Singida, Omar Malule amechaguliwa kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi Mei kutokana na kufanya vizuri katika menejimenti ya matukio ya michezo pamoja na masuala yanayohusu miundombinu uwanjani.

Katika hatua nyingine Salum Mlemwa wa Gunners amechaguliwa Mchezaji Bora waMwezi Mei wa Ligi ya NBC Championship 2025/26, huku Henry Mkanwa pia waGunners akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.

Mlemwa aliyeingia fainali na Richardson Ng’ondya wa Geita Gold na Maulid Shaaban wa Geita Gold, alionyesha kiwango chenye mwendelezo ikiwa ni pamoja na kufunga mabao manne kwa dakika  357  za michezo mitano aliyocheza.

Kwa upande wa Mkanwa aliyeingia fainali na Twaha Beimbaya wa B19 na Mbwana Makata wa Polisi Tanzania, aliiongoza timu yake kushinda michezo yote minne iliyocheza na kupaa kutoka nafasi ya 11 hadi ya saba kwenye msimamo wa Ligi yaChampionship ya NBC.

Pia Kamati ya Tuzo iliteua mabao matatu bora yatakayopigiwa kura na mashabikiili kupata bao bora la mwezi. Mabao hayo ni la Paul Peter (JKT Tanzania vs Fountain Gate dakika ya 85), Clatous Chama (Simba SC vs Young Africans, dakika ya 9) na Christopher Tibandeke (TRA United vs Mtibwa Sugar dakika ya 8).

TAARIFA YA KAMATI YA UENDESHAJI NA UDHIBITI WA LIGI YA BODI YA LIGI KUU TANZANIA (TPLB).

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Juni 8, 2026 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;

Ligi Kuu ya NBC

Mechi Namba 189: TRA United 2-1 Mtibwa Sugar

Mchezaji wa Mtibwa Sugar, Magata Fredrick amefungiwa michezo mitano (5) na kutozwaV faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kurudi uwanjani na kuwa sehemu ya mchezo licha ya kufanyiwa mabadiliko na timu yake.

Magata alifanya tukio hilo Sekunde chache baada ya kufanyiwa mabadiliko na alipoona timu yake ikishambuliwa alirudi uwanjani hivyo kufanya wachezaji wa timu ya Mtibwa kuwa 12. Baada ya shambulio hilo, Magata alitoka nje huku akijificha nyuma ya wachezaji wa timu yake ili asionekane na waamuzi. Kosa hili ni kinyume na kanuni ya17:30 kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 41:5(5.6) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

Klabu ya TRA United imetozwa faini ya Sh. 5,000,000 (milioni tano) kwa kosa la Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Etienne Ndayiragije kutokuhudhuria kwenye mkutano wa waandishi wa habari siku moja kabla ya mchezo bila kutoa taarifa na badala yake alifika kocha msaidizi kinyume na kanuni ya 17:58 kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62 kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 191: Coastal Union 12 Simba SC

Mchezaji wa Coastal Union, Meshack Abraham amefungiwa michezo mitatu (3) kwa kosala kumchezea mchezo usio wa kiungwana (rafu) mchezaji wa Simba Anicet Oura nakuhatarisha usalama wake.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 41:5 Udhibiti kwa Mchezaji.

Mechi Namba 193: TRA United 12 Fountain Gate

Klabu ya TRA United imetozwa faini ya Sh. 11,000,000 (milioni kumi na moja) kwa kosala Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Etienne Ndayiragije kutokuhudhuria kwenye mkutano nawaandishi wa habari siku moja kabla ya mchezo bila kutoa taarifa na badala yake kuwakilishwa na Kocha Msaidizi kinyume na matakwa ya kanuni ya 17:58 kuhusu Taratibu za Mchezo.

Hili ni kosa la kujirudia kwa Kocha huyo ambapo licha ya klabu hiyo kukumbushwa kuhusu utekelezaji wa kanuni hiyo bado kocha huyo hakuhudhuria mikutano hiyo kwenye michezo mitano (5) mtawalia. Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62 kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 197:  Simba SC 1-0 Dodoma Jiji FC

Klabu ya Simba imetozwa faini ya Sh. 5,000,000 (milioni tano) kwa kosa la mtoto muokota mipira kuchukua chupa za maji zilizokuwa pembeni ya goli ya Dodoma Jiji nakumwaga maji yaliyokuwa ndani ya chupa hizo na baadae kuondoka na taulo la mlinda mlango wa Dodoma jiji.

Baada ya mtoto muokota mipira kuondoka na taulo hilo, mlinda mlango huyo na mchezaji Andy Bikoko walimfuata wakimtaka kurejesha taulo hilo, lakini baadhi ya washabiki wa Klabu ya simba waliokua karibu na eneo hilo walianza kurusha chupa zenye vimiminika kwa wachezaji hao wa Dodoma Jiji.

Kitendo hicho cha mtoto muokota mipira kumwaga maji, kuondoka na taulo na washabiki wa Simba kurusha chupa, vinatafsiriwa kutokuwa vya kiungwana.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 47:2 kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

Mshabiki wa klabu ya Simba, Omary Omary (maarufu kwa jina la Bomba) amefungiwa kuingia viwanjani kwa kipindi cha miezi 12 kwa kosa la kufanya fujo kwenye vyumba vyakubadilishia nguo vya timu ya Dodoma Jiji akimtuhumu kiongozi wa Dodoma Jiji aliyekuwa ndani ya chumba hicho na imani za kishirikina.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 47:2 kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

Mechi Namba 199:  Young Africans 3-1 Namungo FC

Mashabiki wa Young Africans, Baraka Shekimweri (maarufu kwa jina la Baraka Yanga) na Abdulrahman Saidi (maarufu kwa jina la Fumau Mshairi) kwa Pamoja wamefungiwa kuingia viwanjani kwa kipindi cha miezi mitatu (3) kwa kosa la kukiuka utaratibu maalumu wa kuketi uwanjani.

Mashabiki hao kwa pamoja wakiwa na tiketi zenye hadhi ya kuketi kwenye jukwaa la VIP B, walilazimisha kwenda kwenye jukwaa lenye hadhi ya VIP A licha ya kuelekezwa na watu wa tiketi kuwa hawana sifa ya kuketi jukwaa hilo, Mashabiki hao waliruka uzio unaotenganisha maeneo hayo na kwenda jukwaa la VIP A kinyume na utaratibu maalumu wa uwanjani hapo.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 47:2 kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

Ligi ya Championship ya NBC

Mechi Namba 206: Mbuni 0-1 TMA 

Klabu ya Mbuni ya Mkoani Arusha imetozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kutokuheshimu ratiba ya mtiririko wa matukio hivyo kuingia uwanjani kwa kuchelewa kinyume na matakwa ya kanuni ya 17:33 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 kuhusu Taratibu za Mchezo

Mchezaji wa Mbuni, Yunus Lema ametozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kukwepa kupeana mikono na timu mgeni kabla ya mchezo ilihali alikuwa sehemu ya kikosi cha kwanza. Yunus alielekea kwenye benchi la timu yake wakati ambao timu mgeni na timu mwenyeji walikuwa wakipeana mikono kabla ya mchezo kuanza.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 41:5(5.4) kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji

Mechi Namba 207: African Sports 1-3 Polisi Tanzania

Klabu ya African Sports ya Mkoani Tanga imepewa adhabu ya onyo kali kwa kosa la kuwakilishwa na wawakilishi wanne (4) badala ya wawakilishi wa tano (5) kwenye kikao cha maandalizi ya mchezo kinyume na matakwa ya kanuni ya 17:2(2.1).Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 kuhusu taratibu za mchezo.