AZAM YATAKATA ARUSHA, KMC IKISHUKA DARAJA.

TIMU ya Azam imetakata katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kuvuna alama tatu na mabao mawili baada ya kuichapa timu ya Fountain Gate katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid .

Mchezo huo uliopigwa saa kumi jioni ulianza kwa timu zote kushambuliana kwani kila timu ilizitaka alama tatu muhimu.

Ilimchukua dakika 36 mshambuliaji wa Azam Jean Ngita kufungua ukurasa wa mabao ambapo timu hiyo ilienda mapumziko ikiwa mbele kwa 0-1.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi Fountain wakitaka kusawazisha ambapo dakika ya 64 mshambuliaji wa Azam Jephte Kitambala aliongeza bao la pili kwa timu yake na hadi mchezo huo unatamatika matokeo ni 0-2.

Mkwakwani Tanga wenyeji Coastal Union waliikaribisha Namungo
ambapo timu zote zilihitaji alama ili kujiweka katika nafasi nzuri na dakika 37 ziliwatosha Coastal kupata bao la kuongoza kupitia mchezaji Robert Savilla kabla ya timu ya Namungo kusawazisha kipindi cha pili dakika ya 62 kupitia mchezaji Geofrey Luzindaze hivyo mchezo kumalizika kwa sare ya 1-1.

Saa mbili usiku KMC ilikuwa na kibarua kizito cha kuikaribisha timu ya TRA katika uwanja wa KMC Complex mchezo ulioanza kwa KMC kuonekana ikizitaka alama tatu muhimu hata hivyo haikuweza kufanikiwa baada ya kukubali kipigo cha 0-1z

Ilimchuka dakika 12 beki wa TRA Chamou Karaboue kuipatia bao timu yake ambalo limebaki kuwa bao pekee kufungwa katika mchezo huo mpaka dakika 90 zilipotamatika na hivyo timu ya KMC kushuka daraja kwani hata ikishinda michezo yake iliyosalia haitaweza kutoka kwenye mstari wa kushuka daraja.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *