Author: Yahaya Abushehe

AZAM HAIKAMATIKI, TANZANIA PRISONS, GEITA ZATAKATA LIGI KUU YA NBC.

LADHA ya Ligi Kuu ya NBC iliendelea leo kwa michezo mitatu iliyochezwa kwenye viwanja vitatu tofauti.

Saa 8:00 mchana Tanzania Prisons walikua wenyeji wa Namungo katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya ambapo mchezo huo ulimalizika kwa Tanzania Prisons kuibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Samson Mbangula dakika ya 42 ya mchezo.

Saa 10:00 jioni Geita Gold waliwaalika Singida FG katika uwanja wa Nyankumbu na Geita kuibuka na ushindi wa bao 1 likifungwa na Mchezaji Valentino Mashaka Kusengama dakika ya 79 ya mchezo.

Mchezo wa mwisho ulizikutanisha Kagera Sugar dhidi ya Azam katika uwanja wa Kaitaba Mkoani kagera na kumalizika kwa Kagera Sugar kukubali kichapo cha mabao 4-0.

Kwa matokeo haya Azam anazidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC akifikisha jumla ya alama 31 huku akiwa amecheza michezo 13 tofauti ya alama nne na Yanga anayeshika nafasi ya pili huku akiwa amecheza michezo 10 .

LIGI KUU YA NBC KUPIGWA MIKOA MITATU TOFAUTI LEO.

 

LIGI KUU ya NBC inaendelea leo kwa michezo mitatu katika mikoa mitatu tofauti baada ya kusimama kwa siku moja.

Mchezo wa kwanza utazikutanisha Tanzania Prisons dhidi ya Namungo katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya saa 8:00 Mchana.

Geita Gold watawaalika Singida FG katika uwanja wa Nyankumbu, Geita saa 10:00 alasiri.

Mchezo wa mwisho utapigwa saa 1:00 usiku Kagera Sugar dhidi ya Azam FC katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.

Kagera anaingia kwenye mchezo huu akiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa mabao matatu dhidi ya Simba huku Azam akiifunga JKT Tanzania kwa mabao 2-1 katika uwanja wa Azam Complex.

COASTAL, DODOMA HAZIKAMATIKI LIGI KUU YA NBC

 

LIGI Kuu ya NBC imeendelea Leo kwa Michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa miwili tofauti.

Mchezo wa mapema saa 10:00 alasiri ulizikutanisha JKT Tanzania dhidi ya Coastal Union katika uwanja wa Azam Complex, Dar na kushuhudia Coastal Union akiibuka na Ushindi wa Bao moja lililofungwa na Maabad Maulid Dakika ya 87 .

Coastal Union imepanda hadi nafasi ya 6 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikifikisha jumla alama 19.

Mchezo wa pili ulizikutanisha Dodoma Jiji dhidi ya Ihefu katika uwanja wa Jamhuri, Dodoma na kumalizika kwa Dodoma kuibuka na ushindi wa bao 1 lililofungwa na mchezaji Yasin Mgaza dakika 55 ya mchezo.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa mchezo nmoja kati ya Mtibwa Sugar na Mashujaa Saa 10:00 alasiri katika uwanja Manungu, Morogoro.

MKUTANO MKUU WA 10 TPLB WAFANYIKA DAR ES SALAAM

Mkutano mkuu wa 10 wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania umefanyika Disemba 8, 2023 kwenye ukumbi wa mikutano wa wa NSSF, Ilala na Mgeni Rasmi akiwa ni Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo nchini Mh. Damas Ndumbaro.

Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa soka akiwemo Katibu Mkuu Mtendaji wa (BMT) Neema Msitha na Katibu Mkuu wa TFF Kidao Wilfred.

Akifungua mkutano huo wa 10 mgeni rasmi, Mh Ndumbaro aliisisitiza Bodi ya Ligi na TFF kuendelea kuweka mikakati madhubuti kuhakikisha ligi kuu inakuwa namba moja Afrika.

Alisema Katika miaka 10 Bodi ya Ligi imefanya mambo mengi mazuri, ikiwa ni pamoja na kutoa ligi katika nafasi ya 10 hadi hadi kuwa ligi ya 5 kwa ubora Afrika huku akiwataka kuweka mkakati wakuifanya iwe namba moja.

Aidha alisema ubora wa ligi kuu ndio umefanya hivi karibuni CAF ikatuamini na kutupatia uwenyeji kwenye ufunguzi wa mashindano mapya ya African Football Leagu na kuwataka watanzania na wadau wa soka kuwasifu, kujivunia pamoja na kuunga mkono utendaji na usimamizi bora kwenye sekta hiyo ya mpira wa miguu.

Kwa upande wa Afisa Mtendaji Mkuu Almasi Kasongo alisema kupitia mkutano huo wanaamini watakwenda kufikia maazimio yaliyopangwa kwa mwaka ujao kama ambavyo taratibu zao zilivyo za kuboresha kila mwaka.

alizitaka timu zote kuzingatia utekelezaji wa udhibiti na ukaguzi wa klabu (club licencing) huku akisisitiza timu hizo kusimamia maeneo yanayounda udhibiti na ukaguzi wa klabu (Club licencing) hasa katika kuimarisha uchumi wa klabu na kudhibiti madeni ambayo yamekuwa yakirudisha nyuma hadhi ya klabu na ligi kwa hatua ya Kitaifa na kimataifa.

Mkutano huo wa 10 wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ulihudhuliwa na viongozi mbalimbali kutoka TFF na Bodi ya ligi pamoja na viongozi waliowakilisha timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya NBC, Ligi ya NBC Championship na First League.

‘LADHA’ ZA LIGI KUU YA NBC KUREJEA LEO

LIGI Kuu ya NBC inarejea Leo Novemba 22 kwa michezo miwili baada ya kusimama kwa siku 13 kupisha kalenda ya FIFA ya michezo ya kimataifa.

Mchezo wa kwanza utazikutanisha Geita Gold inayoshika nafasi ya 15 ikiwa na alama saba dhidi ya JKT Tanzania inayoshika nafasi ya sita ikiwa na alama 14 katika mchezo utakaoanza saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita.

Mchezo wa mwisho hii leo utazikutanisha Kagera Sugar inayoshika nafasi ya nane ikiwa na alama 12 dhidi ya KMC iliyo na alama 15 kwenye nafasi ya tano, saa 1:00 usiku kwenye uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.