TIMU ya Kiluvya ya Mkoani Pwani imefanikiwa kubakia kwenye Ligi ya Championship ya NBC kwa msimu unaofuata baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Transit Camp hivyo kufanikiwa kubaki kwa ushindi wa jumla (aggregate) wa mabao 4-3.

Mchezo wa kwanza uliochezwa wiki iliyopita kwenye uwanja wa TFF Technical Center – Kigamboni Transit Camp iliibuka na ushindi wa mabao 3-2.
Kiluvya iliyopanda daraja kutoka ligi ya First League haikuwa na msimu bora baada ya kumaliza ligi ikiwa imefunga mabao machache (19) sawa na timu ya Cosmopolitan iliyoshuka daraja.
Transit Camp sasa itacheza na Rhino Rangers ya mkoani Tabora kuwania kubakia kwenye Ligi ya Championship ya NBC kwa msimu ujao wa 2025/2026.

Rhino imepata nafasi ya kucheza mchezo huo baada ya kuitoa timu ya Nyumbu kwa tofauti ya mabao 5-3 na itafanikiwa kupanda ligi ya Championship ya NBC ikiwa itaifunga timu ya Transit Camp kwa tofauti kubwa ya mabao kwenye mchezo wa nyumbani na ugenini.
