UTAMU wa Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika unazidi kukolea timu ya Simba ikiichapa timu ya Pamba Jiji kutoka jijini Mwanza mabao 5-1.
Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa KMC uliopo Mwenge mkoani Dar es Salaam ulishuhudia kiungo wa timu ya Simba Jean Ahoua akifunga Mabao matatu (Hat-Trick).
ilimchukua dakika 16 kufungua ukurasa wa mabao kupitia mkwaju wa penati kabla ya kurejea wavuni tena dakika ya 37 hivyo kuifanya timu yake kwenda mapumziko ikiongoza 2-0 dhidi ya Pamba Jiji.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Ahoua aliongeza bao la tatu hivyo kukamilisha hat-trick dakika ya 48 ya mchezo na mshambuliaji Leonel Ateba aliongeza mabao mawili kwa timu yake ikiwa ni dakika ya 80 na 82 ya mchezo huo huku mchezaji wa Pamba Jiji.
Mathew Momanyi alifunga bao la kufutia machozi kwa timu yake ya Pamba dakika ya 86 hivyo mchezo huo kumalizika 5-1.
Ushindi huo unaifanya timu ya Simba kufikisha alama 66 ikiendelea kusalia nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu huku Jean Ahoua akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.