LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa timu ya Singida Black Stars kupata ushindi mnono wa mabao 4–1 dhidi ya Mbeya City ugenini katika mchezo uliochezwa mkoani Manyara kwenye uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara.
Mbeya City ilianza vizuri mchezo na kupata bao la kuongoza dakika ya 14 kupitia kwa mshambuliaji Vitalis Mayanga.
Hata hivyo, Singida Black Stars walirudi kwa nguvu na kusawazisha dakika ya 31 kupitia kwa Emmanuel Keyeh kupitia mkwaju wa penati na kufanya timu hizo kwenda mapumziko zikiwa sare.
Kipindi cha pili kilikuwa cha Singida Black Stars ambapo iliongeza kasi ya mashambulizi na dakika ya 69 Mosi Ndumumwe aliifungia timu yake bao la pili kabla ya beki Ibrahim Imoro kufunga mabao mawili mfululizo dakika ya 72 na 86 na kuhitimisha karamu hiyo ya mabao kwa Singida.
Ushindi huo unaifanya Singida Black Stars kuendelea kujiweka kwenye hali nzuri katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC huku Mbeya City wakilazimika kujipanga upya kwa ajili ya michezo ijayo.
Mchezo mwingine ulipigwa saa 2 :30 usiku katika uwanja wa Benjamin william Mkapa ambapo mabigwa watetezi Young africans waligawana alama na Azam baada ya kutoka sare katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa na kasi kutoka kwa timu zote mbili
Katika mchezo huo kiungo mahiri wa Azam Feisal Salum aliibuka kuwa mchezaji bora wa mchezo huo kufuatia kiwango chake kizuri alichokionyesha uwanjani.