Category: STORY

MASHUJAA, GEITA KUSAKA HESHIMA LIGI KUU NBC

LIGI KUU ya NBC inaendelea leo Novemba 6 kwa michezo miwili kwenye Mikoa miwili tofauti kati ya Mashujaa wakiwaalika Singida BS kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mkoani kigoma na Geita Gold dhidi ya Tabora United kwenye uwanja wa Nyankumbu, Geita huku michezo yote ikianza saa 10:00 alasiri.

Mashujaa wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza michezo mitatu mfululizo ya Ligi Kuu ya NBC.

Geita Gold inashika nafasi ya 15 kwenye msimamo baada ya kucheza michezo minane ikishinda mmoja, ikisuluhu michezo mitatu na kufungwa mitano hivyo kukusanya alama sita.

Tabora United ipo nafasi ya nane ikishinda michezo miwili,
sare michezo minne na kufungwa mitano hivyo kuwa na alama 10 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

YANGA YAIADHIBU SIMBA LIGI KUU YA NBC.

MABAO 5-1 walioshinda Yanga dhidi ya Simba yametosha kuwabakiza kileleni mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya NBC kwa alama 21 baada ya kucheza mechi tisa.

Mabao yaliyofungwa na Kennedy Musonda, Maxi Nzengeli aliyefunga mawili, Ki Aziz na Pacome Zouzoua yameifanya Simba kuruhusu mabao 10 huku wakifunga 17.

Ushindi huo umeifanya Yanga kufikisha jumla ya mabao 25 kwenye michezo 9 waliyocheza mpaka sasa.

Yanga wamesalia kileleni mwa msimamo wakiwaacha wapinzani wao Simba na pointi zao 18 huku Simba wakiwa wamecheza mechi saba .

KMC NDANI YA TATU BORA LIGI KUU YA NBC.

 

LIGI KUU ya NBC imeendelea Leo kwa Mchezo mmoja katika uwanja wa Uhuru, Dar na kushuhudia KMC akiibuka na Ushindi wa Bao moja dhidi ya Mtibwa Sugar, lililowapeleka mpaka nafasi ya tatu ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Bao pekee na la ushindi kwa KMC limefungwa na Ibrahim Elias Dakika ya 15 ya mchezo na kuifanya KMC kufikisha alama 15 na michezo saba mfululizo bila kupoteza.

Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo mitatu, mapema saa 8:00 Mchana Singida BS watawaalika Ihefu katika uwanja wa Liti mkoani Singida, Mashujaa watawaalika Azam FC saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma na Mchezo wa mwisho saa 1:00 usiku Coastal Union watakuwa wenyeji wa Namungo katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.

AZIZ KI KINARA WA MABAO LIGI KUU YA NBC.

MCHEZAJI Stephane Aziz Ki wa Yanga amemshusha Jean Baleke wa Simba kwenye msimamo wa vinara wa mabao baada ya kufunga mabao matatu (Hat-trick) dhidi ya timu ya Azam.

Mabao matatu aliyofunga Ki yote kwa mguu wa kushoto yamemfanya kufikisha mabao sita na kumzidi Baleke mwenye matano na Feisal Salum wa Azam mwenye mabao manne.

Matokeo hayo yanaifanya Yanga kufikisha alama 15 sawa na timu ya Simba na kupanda nafasi ya kwanza kwa tofauti ya mabao manne.

Ligi Kuu ya NBC itaendelea tena Oktoba 25 kwa michezo mitatu, JKT Tanzania dhidi ya Tabora United kwenye uwanja wa Azam Complex saa 16:00, Coastal Union na Mashujaa saa 12:30 kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga na mchezo wa mwisho utachezwa uwanja wa Jamhuri saa 21:00 kati ya Dodoma Jiji na Kagera Sugar.

‘KIVUMBI’ DAR ES SALAAM DERBY LIGI KUU NBC.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo ikikutanisha ‘miamba’ wawili wa soka kutoka mkoa wa Dar timu ya Yanga dhidi ya Azam kwenye uwanja wa Mkapa, Dar utakaochezwa saa 12:30 jioni.

Yanga ndiye kinara wa kufunga mabao mpaka sasa (15) huku akiruhusu mabao mawili sawa na Azam.

Azam imeshinda michezo minne mpaka sasa na kutoa sare mmoja ikiwa haijapoteza mchezo wowote huku Yanga ikishinda minne na kupoteza mmoja.

Yanga imeshinda michezo mitano huku Azam ikishinda mitatu na sare tatu zimepatikana miamba hiyo ilipokutana kwenye michezo 10 iliyopita.