Category: STORY

HAWA HAPA VINARA WA MABAO NBC CHAMPIONSHIP.

 

Jumla ya mabao 329 yameshafungwa katika michezo 144 sawa na mizunguko 18 ya Ligi ya NBC Championship mpaka kufikia sasa.

Edger William wa KenGold ndiye kinara wa upachikaji mabao ndani ya Ligi ya NBC Championship akifunga mabao 15 huku timu yake ikifunga mabao 32.

Boban Bogere wa Biashara United ndiye anayefuatia akifunga mabao 13 kwenye mabao 32 yaliyofungwa na timu yake.

Ramadhani kapera aliyekuwa Mbeya Kwanza kabla ya kutimkia Geita Gold inayoshiriki Ligi Kuu ya NBC na Salim Aiyee aliyekuwa timu ya Mbuni kabla ya kujiunga na Coastal Union ya Ligi Kuu ya NBC wanafuata kila mmoja akifunga mabao 9.

KENGOLD YAREJEA KILELENI, NBC CHAMPIONSHIP IKIENDELEA LEO.

 

LIGI ya NBC Championship imeendelea leo Januari 21 kwa michezo mitatu kupigwa kwenye mikoa mitatu tofauti.

Mchezo wa mapema saa 8:00 mchana ulizikutanisha TMA dhidi ya Cosmopolitan kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2.

Mkoani Mwanza Copco ikawakaribisha Biashara United kwenye uwanja wa CCM Kirumba saa 10:00 alasiri na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Mchezo wa mwisho kwa leo ulizikutanisha KenGold dhidi ya Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya na kumalizika kwa KenGold kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Ushindi wa KenGold unairejesha kwenye uongozi wa msimamo wa Ligi ya NBC Championship baada ya kufikisha alama 42 kwenye michezo 18.

NBC CHAMPIONSHIP MECHI ZOTE MUBASHARA KUPITIA TV3.

 

MECHI zote za Ligi ya NBC Championship sasa zitarushwa mubashara na mdhamini mwenye haki ya matangazo TV3.

TV 3 ambayo inapatikana kwenye chaneli namba 197 (dish) na 137 (antena) kwenye king’amuzi cha Startimes, awali ilikuwa ikirusha baadhi ya michezo lakini baada ya maboresho ya ratiba sasa michezo yote kuonekana mubashara kupitia chaneli hiyo.

Hii ni hatua kubwa kwa Ligi ya NBC Championship kwani vipaji lukuki vilivyopo huku vitakuwa na nafasi ya kuonekana kwa ukubwa zaidi ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

NBC CHAMPIONSHIP HAKUNA MBABE LEO.

 

MICHEZO miwili ya mzunguko wa 18 ya Ligi ya NBC Championship imechezwa leo na michezo yote kumalizika kwa sare.

Mchezo wa kwanza ulizikutanisha Polisi Tanzania dhidi ya Green Warriors saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa ushirika, Kilimanjaro na kumalizika kwa suluhu.

Saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro FGA Talents ikaikaribisha Transit Camp na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2 .

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa michezo mitatu kupigwa Mbuni itawakabili Pan African, Pamba dhidi ya Stand United na Mbeya City dhidi ya Mbeya Kwanza.

KILIMANJARO, MOROGORO KUSHUHUDIA NBC CHAMPIONSHIP LEO.

 

Mzunguko wa 18 wa Ligi ya NBC Championship unaanza leo Januari 19 kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa miwili tofauti.

Mkoani Kilimanjaro Polisi Tanzania watawaalika Green Warriors saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa Ushirika.

Saa 10:00 alasiri FGA Talents itakuwa mwenyeji wa Transit Camp kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.

FGA Talents na Transit Camp zinapambana kujinasua kutoka nafasi za mwisho kwenye msimamo ambapo FGA Talents imekusanya alama 15 kwenye michezo 17 ikiwa kwenye nafasi ya 12 huku Transit Camp ikikusanya alama 14 kwenye michezo 17 ikiwa na nafasi ya 14.