Category: TAARIFA

TAARIFA YA KAMATI YA USIMAMIZI WA LIGI YA BODI YA LIGI KUU

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Februari 21, 2025 ilipitia mwenendo na matukio ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;

Ligi Kuu ya NBC

Mechi Namba 140: Mashujaa FC 0-0 Coastal Union

Klabu ya Mashujaa ya Kigoma imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kuingia uwanjani kwa kutumia mlango usio rasmi kinyume namatakwa ya Kanuni ya 17:21 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo, na kusababisha mdhamini mwenye haki yamatangazo ya runinga, Azam Media Limited kushindwakupata picha za tukio la timu kuwasili. Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 147: JKT Tanzania 0-1 Singida BS

Klabu ya Singida BS imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kutokutumia chumba maalumu cha kubadilishia nguo, kinyume na matakwa yaKanuni ya 17:20 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 150: Tabora United 1-1 KenGold

Klabu ya Tabora United imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 2,000,000 (milioni mbili) kwa kosa la wawakilishi watimu hiyo kufika kwenye kikao cha maandilizi ya mchezo bila kifaa chochote kinyume na matakwa ya kanuni ya17:2(2.2) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:(2.2 & 62) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 151: Azam FC 2-0 Mashujaa FC

Klabu ya Mashujaa ya imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kuchelewakurejea kiwanjani baada ya muda wa mapumziko kumalizika. Mashujaa walichelewa kutoka vyumbani kwa dakika tano (5) jambo lililosababisha kuchelewa kuanzakwa kipindi cha pili.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:(33 & 62) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mchezaji Seif Karihe wa Mashujaa ameadhibiwa kwa kufungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa Azam FC, Feisal Salum. Karihe alimkanyaga Feisal wakati akiwa chini baada ya kumfanyia rafu.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 41:5 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

Mechi Namba 155: Namungo FC 0-3 Simba SC

Mchezaji wa Namungo Daniel Amoah ameadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuonekana akimwaga vimiminika kwenye goli jambolililohusianishwa na vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina.Amoah alionekana akifanya tukio hilo wakati timu ya Simba ikijiandaa kupiga penati.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 41:3 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

TAARIFA

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imefuta adhabuya kadi nyekundu kwa mchezaji wa Namungo, Derick Mukombozi aliyoadhibiwa na mwamuzi wa mchezo tajwahapo juu. Kamati imefikia maamuzi hayo baada ya kujiridhisha kuwa maelezo yyaliyopo kwenye ripoti yamwamuzi hayana ushahidi wa kutosha unaoendana namarejeo ya picha mjongeo.

Mechi Namba 157: Mashujaa 2-0 Pamba

Klabu ya Mashujaa ya mkoani Kigoma imeadhibiwa kwakupewa onyo kali kwa kosa la Watoto waokota mipira (ball kids) kuchelewa kwa makusudi kurejesha mipira uwanjanikwa wakati. Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:48 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za mchezo.

Mchezaji wa klabu ya Pamba Jiji ya Mwanza, KassimSuleiman ameadhibiwa kwa kufungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kumpiga kwa kutumia mpira ‘Ball Kid’ baada ya kukaa nampira huo muda mrefu bila kuurejesha kiwanjani. Mchezaji huyo aliadhibiwa kwa kadi nyekundu pia na mwamuzi wa mchezo kwa kosa hilo Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 41:5 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

Mechi Namba 159: Young Africans 2-1 Singida BS

Klabu ya Young Africans imeadhibiwa kwa kupewa onyo kali kwa kosa la viongozi wake kuingia kwenye eneo la kuchezea (pitch area) baada ya mchezo tajwa hapo juukukamilika.

Viongozi hao wa klabu ya Yanga walioingia uwanjani walisababisha kukosekana kwa utulivu wakati wamahojiano ya mdhamini mwenye haki za matangazo yaruninga.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:50 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 160: KenGold 1-0 Kagera Sugar

Klabu ya KenGold imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la maafisa wake kuchelewa kuwasili kwenye kikao cha maandalizi ya mchezo (MCM). Maafisa hao walifika kwenye kikao saa 4:30asubuhi badala ya saa 4:00 asubuhi kinyume na matakwaya Kanuni ya 17:2(2.2) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Ligi ya Championship ya NBC

Mechi Namba 151:  Stand United 2-1 TMA

Klabu ya TMA imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kuharibu uzio wauwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga. TMA walifanya uharibifu huo ili wachezaji wao wapite chini ya uzio badala ya kupita kwenye mlango rasmi.

TMA walitumia eneo hilo la uzio lililoharibiwa kwa kuingiakiwanjani wakati wa kupasha misuli moto, wakati wakwenda kuanza kwa mchezo, wakati wa mapumziko nabaada ya mchezo kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:21 ya Ligi ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62 ya Ligi yaChampionship kuhusu Taratibu za Mchezo.

TAARIFA KUTOKA BODI YA LIGI TANZANIA

KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Disemba 1, 2022 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;

 

Ligi Kuu ya NBC (NBCPL)

Mechi Namba 37: Mbeya City FC 1-1 Simba SC

Timu ya Simba imetozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la baadhi ya wachezaji wake kuingia uwanjani kwa kupitia mlango usio rasmi kuelekea mchezo tajwa hapo juu uliofanyika kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya Novemba 23, 2022.

Simba walilazimisha baadhi ya wachezaji wao waruhusiwe kuingia uwanjani kupitia mlango wa kuingilia jukwaa la watu maalum na walipozuiwa na walinzi wa uwanjani (stewards), Simba walitumia nguvu kutimiza nia yao.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:(21 & 60) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

Mchezaji wa timu ya Simba, Gadiel Michael amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kulazimisha kuingia uwanjani saa 4:25 asubuhi ya siku ya mchezo tajwa hapo juu kwa kile alichoeleza alitaka kukagua kiwanja.

Licha ya walinzi wa uwanja huo kumzuia Gadiel (ambaye alikuwa ameongozana na watu kadhaa waliovalia fulana zenye nembo ya klabu ya Simba), kwasababu haukuwa muda rasmi kwa ajili ya zoezi hilo na Simba hawakufanya mawasiliano yoyote na Kamishna wala Mratibu wa Mchezo wakieleza jambo hilo, Gadiel alitumia hila na kufanikiwa kuwakwepa walinzi hao kisha kuingia kiwanjani.

Mchezaji huyo alipoingia kiwanjani hakuonesha dalili yoyote ya kukagua eneo la kuchezea na badala yake alionekana kwenda moja kwa moja hadi eneo la katikati ya kiwanja na kumwaga vitu vyenye asili ya unga.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni 41:5(5.5) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti kwa Wachezaji.

 

Kamati imeikumbusha Timu ya Mbeya City kuhakikisha viongozi wake waliofungiwa wanatekeleza adhabu zao kikamilifu ikiwemo kutojihusisha na masuala ya timu hiyo hadi pale adhabu zao zitakapomalizika.

Katika mchezo tajwa hapo juu, kiongozi wa Mbeya City, Frank Mfundo ambaye anatumikia adhabu ya kufungiwa, alionekana kufanya kazi za klabu hadi pale walipomuondoa kwa haraka baada ya kuelezwa juu ya jambo.

Klabu ina wajibu wa kuhakikisha viongozi na wachezaji wao walioadhibiwa wanatekeleza masharti ya adhabu zao kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni ya 47:5 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

 

Timu ya Mbeya City imetozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la baadhi ya viongozi wake kumtolea lugha chafu Mratibu Msaidizi wa Mchezo tajwa hapo, wakilazimisha kuingia katika eneo la kimashindano mara baada ya mchezo kumalizika na wakati makochwa wa timu zote mbili wakiendelea kuhojiwa na Azam TV.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:(21 & 60) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mchezo tajwa hapo juu ulikuwa na mapungufu katika uamuzi hivyo Kamati imepeleka shauri la waamuzi wa mchezo huo kwenye Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu, TFF kwa ajili kujadiliwa na kutolewa ushauri wa kitaalamu kabla ya kufanyika kwa maamuzi.

 

Mechi Namba 38: Ihefu SC 2-1 Young African SC

Kocha wa timu ya Young African, Nasreddine Nabi amefungiwa michezo mitatu na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuwashambulia kwa maneno mwamuzi wa kati na mwamuzi wa akiba wa mchezo tajwa hapo juu.

Kocha Nabi aliendelea kufanya kitendo hicho hata baada ya kuonywa kwa kadi ya manjano.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 42:2(2.1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Makocha.

 

Mechi Namba 106: Ruvu Shooting FC 0-1 Singida Big Stars FC

Klabu ya Ruvu Shooting imetozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuchelewa kuwasili uwanjani kuelekea mchezo tajwa hapo juu.

Ruvu Shooting waliwasili uwanjani saa 8:42 mchana badala ya saa 8:30 mchana kama ilivyoainishwa kwenye kanuni ya 17:15 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:60 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

Mechi Namba 109: Polisi Tanzania FC 1-3 Simba SC

Klabu ya Polisi Tanzania imetozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuingia uwanjani kwa kupitia mlango usio rasmi kuelekea mchezo tajwa hapo juu uliofanyika kwenye uwanja wa Ushirika uliopo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, Novemba 27, 2022.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:(21 & 60) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

Mechi Namba 110: Azam FC 3-2 Coastal Union FC

Mchezaji wa klabu ya Coastal Union, Maabadi Maabadi amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kumshambulia mwamuzi wa kati wa mchezo tajwa hapo juu kwa kumrushia chupa ya maji na baadaye kiatu.

Mchezaji huyo ambaye alikuwa kwenye benchi baada ya kufanyiwa mabadiliko, alionekana akiingia kiwanjani na kumrushia chupa mwamuzi wa kati wakati mchezo ukiendelea kisha kwenda kumshambulia mwamuzi huyo kwa kutumia kiatu baada ya mchezo kumalizika.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 41:5(5.3) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

 

Klabu ya Coastal Union imetozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la baadhi ya wachezaji wake na viongozi wa benchi la ufundi kurusha chupa za maji kiwanjani wakati mchezo ukiendelea.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 47:1 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

 

Klabu ya Azam imetozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la shabiki wake aliyekuwa ameketi kwenye jukwaa la watu maalum, kurusha chupa ya maji kwa hasira katika eneo hilo mara baada ya timu ya Coastal Union kupata bao la kusawazisha katika mchezo tajwa hapo juu uliomalizika kwa Azam kupata ushindi wa mabao 3-2.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 47:1 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

 

Kamati imepeleka shauri la waamuzi wa mchezo tajwa hapo juu kwenye Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu, TFF kwa ajili kujadiliwa na kutolewa ushauri wa kitaalamu kabla ya kufanyika kwa maamuzi.

 

Ligi ya Championship

Mechi Namba 86: Pan Africans FC 2-0 Biashara United FC

Klabu ya Pan Africans imepewa onyo kwa kosa la kuwakilishwa na maafisa pungufu kwenye kikao cha maandalizi ya mchezo (MCM).

Pan Africans iliwakilishwa na maafisa wanne (4) badala ya watano (5) walioainishwa kikanuni.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:2(2.2) na 17:60 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

Imetolewa na;

Idara ya Habari na Mawasiliano

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB)

Disemba 2, 2022

 

TAARIFA KUTOKA BODI YA LIGI KUU TANZANIA

KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Novemba 25, 2022 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;

 

Ligi Kuu ya NBC (NBCPL)

Mechi Namba 53: Singida Big Stars FC 1-1 Simba SC

Mchezaji wa timu ya Singida Big Stars, Shafiq Batambuze amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuingia kiwanjani kuanza kupasha moto misuli dakika 10 kabla ya muda ulioainishwa kwenye ratiba ya matukio ya mchezo.

Mchezaji huyo alipinga maelekezo ya Mratibu wa Mchezo (GC) na Kamishna wa Mchezo waliomtaka arejee chumbani hadi muda uliopangwa utakapowadia. Akiwa kiwanjani, Shafiq Batambuze alionekana kumwaga vitu kwenye majani jambo lililoashiria imani za kishirikina.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni 41:5(5.5) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti kwa Wachezaji.

 

Kamati imewafungia michezo mitatu na kuwatoza faini ya Sh. 1,000,00 (milioni moja) kila mmoja, Kocha Msaidizi wa Singida Big Stars, Mathias Lule na Kocha wa Makipa wa timu hiyo, Steven Kiagundu kwa kosa la kumuamuru Shafiq Batambuze aendelee kusalia kiwanjani hata pale mchezaji huyo alipojaribu kuondoka.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 45:2(2.4) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Makocha.

 

Timu ya Singida Big Stars imetozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kushindwa kuhudhuria Mkutano wa Wanahabari uliopangwa kufanyika Novemba 8, 2022 kwenye ukumbi wa Benki ya NBC tawi la Singida, kuelekea mchezo tajwa hapo juu.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:(56 & 60) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

 

Mechi Namba 94: Ihefu SC 1-2 Polisi Tanzania FC

Kamati imemfungia miezi mitatu (3) na kumtoza faini ya Sh. 500,000 (laki tano), Afisa Usalama wa klabu ya Polisi, Nelson Ngonyani kwa kosa la kumshambulia kwa matusi Mratibu wa Mchezo tajwa hapo juu, akipinga maelekezo halali yanayohusu kufuata taratibu za mchezo.

Afisa Usalama huyo aliendelea kwa kumtaka Mratibu wa Mchezo husika akashtaki kwenye mamlaka yoyote kwani anajua hakuna anayeweza kumfanya chochote.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 46:3 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Viongozi.

 

Mechi Namba 104: Dodoma Jiji FC 0-2 Young Africans SC

Timu ya Young Africans  imepewa onyo kwa kosa la kuchelewa kuwasili kwenye Mkutano wa Wanahabari (Pre-Match Press Conference) kwa dakika 35.

Kocha Mkuu na nahodha au mchezaji mwenye ushawishi kikosini wanapaswa kushiriki mkutano wa Wanahabari siku moja kabla ya mchezo na katika muda uliopangwa kwenye ratiba ya mikutano hiyo.

Yanga walifika ukumbini saa 7:05 mchana badala ya saa 6:30 mchana.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:(56 & 60) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

Kamati imeionya timu ya Dodoma Jiji kwa kosa la viongozi wake kuingia katika chumba cha kuvalia wachezaji wa timu hiyo ndani ya muda wa kikanuni wa mchezo.

Viongozi hao walishuka kutoka jukwaani wakati wa mapumziko na kuingia ndani ya chumba hicho, kitendo ambacho ni kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:17 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:60 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

MUHIMU

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imepeleka mashauri yote ya waamuzi kwenye Kamati ya Waamuzi ya TFF kwa ajili ya uchambuzi wa kitaalamu wa maamuzi yote yenye utata yaliyofanyika kwenye michezo ya Ligi Kuu ya NBC, kabla ya kurejeshwa kwa ajili ya kujadiliwa na kutolewa maamuzi na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi.

Ligi ya Championship

Mechi Namba 65: Biashara United FC 2-1 Kitayosce FC

Timu ya Biashara United imetozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la mashabiki wake kutoa vitisho na lugha ya matusi kwa waamuzi wa mchezo tajwa hapo juu kabla ya kuanza kwa mchezo.

Mashabiki hao waliendelea kufanya vitendo visivyo vya kimchezo kwa kurusha mawe juu ya paa la chumba cha waamuzi wakitoa kauli za vitisho kuwa waamuzi hao wasingetoka salama uwanjani hapo kama timu yao isingepata matokeo ya ushindi katika mchezo huo.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 47 ya Championship kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

 

MUHIMU

Kamati imeitaka klabu ya Biashara United kuhakikisha vitendo vya namna hii havijirudii tena kwenye uwanja wao kwani vikijirudia, hatua kali zaidi za kikanuni zitachukuliwa ikiwemo kuzuia mashabiki kuingia uwanjani katika michezo yake yote au kuufungia uwanja Karume kutumika kwa michezo ya Ligi.

 

Mechi Namba 72: Gwambina FC 2-4 Ndanda FC

Klabu ya Gwambina imetozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuchelewa kufika uwanjani kwa dakika 38.

Gwambina ilifika kwenye uwanja wa Nyamagana saa 9:08 alasiri badala ya saa 8:30 mchana kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni ya 17:15 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.

Adhabu hiyo ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:60 ya Championship kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

 

Mechi Namba 73: Gwambina FC 2-1 Mashujaa FC

Klabu ya Gwambina imetozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuchelewa kufika uwanjani kwa dakika 75.

Gwambina ilifika kwenye uwanja wa Nyamagana saa 9:45 alasiri badala ya saa 8:30 mchana kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni ya 17:15 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.

Adhabu hiyo ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:60 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 76: Mbuni FC 0-1 JKT Tanzania FC

Klabu ya Mbuni imetozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la mashabiki wake wakiongozwa na Katibu wa klabu hiyo, Michael Yoen kuwashambulia waamuzi baada ya kumalizika kwa mchezo tajwa hapo juu kwenye uwanja wa Aga Khan jijini Arusha.

Adhabu hiyo ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 47 ya Championship kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

 

Kamati imemfungia miezi sita (6) na kumtoza faini ya Sh. 2,000,000 (milioni mbili) katibu wa Mbuni FC, Michael Yoen kwa kosa la kuongoza mashabiki kuwashambulia waamuzi na kuendelea kuwafuatilia waamuzi hao hadi hotelini walikofikia.

Adhabu hiyo ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 46:3 ya Championship kuhusu Udhibiti kwa Viongozi.

 

Kamati imempongeza Afisa Usalama wa Chama cha Mpira wa miguu mkoa wa Arusha (ARFA), Mike Warioba kwa juhudi zake za kuhakikisha waamuzi na Kamishna wa mchezo huo hawapati madhara zaidi kutokana na vurugu za mashabiki hao.

Mike Warioba aliwaondoa maafisa hao hotelini na kwenda kuwapa hifadhi katika kituo kikuu cha polisi Arusha kabla ya kuwatafutia usafiri wa kuwaondoa jijini Arusha usiku huo huo wa Novemba 19, 2022.

 

First League

Mechi Namba 14B: Stand United FC 2-0 Kasulu FC

Klabu ya Kasulu imepewa onyo kali kwa kosa la kuwakilishwa na maafisa pungufu kwenye kikao cha maandalizi ya mchezo (MCM).

Kasulu iliwakilishwa na maafisa wawili (2) badala ya watano (5) walioainishwa kikanuni.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 18:2(2.2) na 18:60 ya First League kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

Mechi Namba 19B: Kasulu FC 1-3 Rhino Rangers FC

Klabu ya Kasulu imepewa onyo kali kwa kosa la kuchelewa kufika uwanjani kwa dakika 80.

Kasulu ilifika kwenye uwanja wa Nyamagana saa 9:50 alasiri badala ya saa 8:30 mchana kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni ya 17:15 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.

Adhabu hiyo ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 18:(15 & 60) ya First League kuhusu Taratibu za Mchezo.

 

Kuhusu Klabu ya Njombe Mji

Bodi ya Ligi imepokea barua ya klabu ya Njombe Mji ya mkoani Njombe wakiomba kujitoa kushiriki First League msimu huu wa 2022/2023 baada ya na kukumbwa na matatizo ya kifedha, hali iliyosababisha timu hiyo ishindwe kumudu gharama za kushiriki ligi hiyo.

Kutokana na ombi hilo, Klabu ya Njombe Mji haitoendelea kushiriki First League msimu wa 2022/2023, imeshushwa daraja na kufungiwa kucheza Ligi kwa misimu miwili (2).

Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 31:4(4.1) ya First League kuhusu Kujitoa.

Kwasababu idadi ya michezo ambayo Njombe Mji imecheza hadi kujitoa kwake haizidi nusu ya michezo yote, matokeo ya michezo yote iliyocheza yamefutwa kwa mujibu wa Kanuni ya 31:4(4.3) ya First League kuhusu Kujitoa.

 

Imetolewa na;

Idara ya Habari na Mawasiliano

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB)

Novemba 26, 2022

WANAHABARI WATAKAOHUDHURIA SEMINA YA KUWAJENGEA UWEZO

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeandaa Semina ya siku moja ya kuwajengea uwezo Wanahabari wanaoandika habari za michezo (hasa mpira wa miguu).

Semina hiyo itafanyika kuanzia saa 2:00 asubuhi Jumatatu Agosti 29, 2022 kwenye ukumbi wa mikutano uliopo ghorofa ya kwanza, Jengo la NSSF (Mafao House) lililopo Ilala Boma mkoani Dar es Salaam.

Ifuatayo ni orodha ya Wanahabari watakaohudhuria Semina hiyo ambayo itatanguliwa na zoezi la usajili na kupata kifungua kinywa kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 1:50 asubuhi;

Na JINA CHOMBO CHA HABARI
1 ABDALLAH HAMISI ZEZE INK MEDIA TZ
2 ABDUL MIKIDADI UHURU FM
3 ABDURAHMAN JUMANNE UHURU PUBLICATIONS LIMITED
4 ABUBAKARI MKOBA MUUNGWANA BLOG & TV
5 ABUU RAMADHANI ALLY AYUZA TV
6 ABUU RAMADHANI MWAKYOMA SUPA TV
7 ABUUBAKARI SAID WASAFI MEDIA
8 ALBERT MRINGO MPENJA TV
9 ALFA SIASA ASPORT TZ
10 ALFRED KAVISHE TBC
11 ALHAJI ZUBERI RAJABU MKULE TV
12 ALLY SUKEIMAN MZURI MZURI TV
13 ALUMANUS JULIUS MWASENGA YO! FAVE TV
14 AMANI JOVIN NDIMBO ACTIVE MEDIA
15 AMEDEUS VICTOR SOMI GANGANA INFO CHANNEL
16 AMINA YUSUPH CFM
17 ASHA KIGUNDULA TANZANIA LEO
18 BADI MCHOMOLO TIMES RADIO FM
19 BAKARI KAGOMA BOIPLUS TV
20 BARAKA SILVANUS KIDANI STARS
21 CHRISTIANI MALIBATE C SPORT MEDIA
22 CLECENCE KUNAMBI DAILY NEWS
23 CLEMENT JOHN HITS FM – ZANZIBAR
24 CLEZENCIA TRYPHONE MWANANCHI & MWANASPOTI
25 CLINTON EPIMACK JR MTITA TV
26 COSMASY CHOGA SPORTS STAR TZ
27 CYPRIAN EMMANUEL KASHETO TV3
28 DALIDALI RASHID CLOUDS MEDIA
29 DAMIAN DENIS THEOBALD CLASSIC FM
30 DAUDI YASSIN NABWERA NYIRO TV
31 DAUKA ABRAHAM SOMBA DAR24 MEDIA
32 DAVID NELSON SHIJA MZEE WA MIKITO
33 DAVID PASCHAL SIBUKA MEDIA LIMITED
34 DERICK DAVID KAHIMBA KABUMBU TV
35 DIANA JOHN SONGA BOIPLUS TV
36 DICKSON BISARE MOGENDI MATUKIO DAIMA TV
37 DICKSON R. MASANJA DAUDA TV (ONLINE)
38 DIDAS OLANG JFIVE TV ONLINE
39 DISMAS HILARY ACTIVE MEDIA
40 EDGAR JOHN KIBWANA CLOUDS MEDIA
41 ELISHA PIUS YOHANA REAL MEDIA
42 ELIZABETH JOHN UHURU MEDIA GROUP
43 EMESTO ELIUD SIMKWAI JFIVE MEDIA
44 ESTER FRANCK LEMA AYOMA TV
45 FADHILI OMARY SIZYA DIZZIM FM MOROGORO
46 FARHAN KIHAMU CLOUDS MEDIA
47 FARIDI MIRAJI TBC
48 FATUMA RASHID MBELWA PLUS RADIO
49 FELIX JASON SOKAONLINE
50 FRADIUS MUGOA TBC
51 FREDRICK NWAKA TBC
52 FURAHA RAJABU CHABRUMA JR MTITA TV
53 GERVAS MAKASI JOHN MPENJA TV
54 GIDEON NJONANJE BONA TV
55 GODFREY NYANTO TBC FM
56 GRACE MILANZI MAXIMUM TV
57 GRACE MKOJERA HABARILEO
58 HAJI N SAMRI CLOUDS MEDIA GROUP
59 HAMIS SELEMAN MAHURUKU HITS FM DAR ES SALAAM
60 HAMZA FUMO BONGO5 MEDIA GROUP LTD
61 HASSAN DAUDI DIMBANI
62 HONEST AMON MWANITEGA FREELANCER
63 HUMPHREY MSECHU SPARKLIGHT TV
64 HUSEIN MOHAMED GLOBAL TV
65 HUSEIN SHAFII TBC
66 HUSSEIN MIRAJI MCHOMVU LAXY TV
67 IBRAHIM LOITORE SIKON MWANANCHI & MWANASPOTI
68 IBRAHIM MUSSA GLOBAL PUBLISHERS
69 IBRAHIM THABIT SANGA SUPA TV
70 INNOCENT OKAMA TFF MEDIA
71 ISAACK WAKUGANDA MUST FM RADIO
72 ISIKE PETER FRED SUPA TV
73 ISMAIL HUSSEIN MWAMBA MWAMBAFIVE (ONLINE TV)
74 ISSA SALUMU LIPONDA GLOBAL PUBLISHERS
75 JACKSON SILLO ITV / RADIO ONE
76 JAMES ABLE BONA TV
77 JAMES JOSEPH RANGE TBC
78 JAMILLA KASSIMU WRM TV
79 JAPHARY LESSO LONGA TV
80 JOHN MACHELA MASHUJAA FM
81 JOHN MAGANGA TV3
82 JOHN RICHARD MARWA SIBUKA FM
83 JOSEPH BENEDICTOR KESSY TIMES FM RADIO
84 JOSEPH SOPOLA DAVID HABARI FM, ZANZIBAR LEO
85 JUMA BAKARI KINANGUKA ZENJ FM
86 JUMANNE MAKAMBI KINGO BOIPLUS TV
87 KALUNDE MAHIMBO SAID TBC
88 KHATIMU AHMEID NAHEKA MWANANCHI
89 KUSHOKA JOSEPH MISHPLUS TV
90 LATIFA MSABAHA TVE TANZANIA
91 LEONARD SYLVESTER NYONI STAR TV
92 MALYO CHETO NJEDENGWA TBC
93 MAREGES NYAMAKA REDIO FREE AFRICA
94 MARTHA MBOMA GLOBAL GROUP
95 MARTIN MAZUGWA HABARI LEO
96 MBWANA SHOMARI STAR TV
97 MEMORASIA SYLVESTER LAXY TV
98 MICHAEL NYANKONGO VALOR TV
99 MOHAMED AKIDA HABARI LEO
100 MOHAMMED ALLY BALHABOU KASI MEDIA
101 MOHAMMED MDOSE HABARI LEO (TSN)
102 MSHAMU HASSAN CLASSIC FM
103 MSHAMU NGOJWIKE WANANCHI SPOTI
104 MUHSINI ABU KIMONJE WALLENIVO MEDIA
105 MWINYIMVUA NZUKWI ZANZIBAR LEO/ZANZIBAR MAIL
106 NASRA KITANA UHURU PUBLICATIONS LIMITED
107 NASSIB MKOMWA ATHUMANI CLOUDS MEDIA
108 NAZARETH JOSEPH UPETE TBC
109 NICKSON SYLVANUS BONFACE AYOMA MEDIA
110 NOEL RUKANUGA FULL SHANGWE TV
111 OMARY MDOSE GLOBAL PUBLISHERS
112 OSCAR N NKEMBO MPENJA TV
113 PATRICK DERRICK MWANKALE AM24 RADIO
114 PATSON MWITA AMSHA MEDIA
115 PETER LUGENDO JOHN TBC FM
116 PETER LUSSE BM TV TANZANIA
117 PETER MAVALA MAVALA TV
118 PHILIP N NYITI CLOUDS MEDIA
119 POLYCARP CLAUDIO MKAI TV
120 QUDRA KAIZA QTV TANZANIA
121 RAHEL JAPHET PALLANGYO TSN LTD
122 RAMADHAN ELIAS MWANANCHI COMMUNICATIONS LIMITED
123 RAMADHANI KAEMBA HTM NEWS
124 RICHARD DEOGRATUS SOMBI MTANZANIA DIGITAL
125 ROBERT RICHARD AMGL
126 SAADA AKIDA IPP MEDIA – NIPASHE
127 SAID ALLY GLOBAL PUBLISHERS
128 SAID ALLY MWANDIKE WAPO RADIO FM
129 SALUM BAKARI KAORATA BM TV TANZANIA
130 SHUFAA LYIMO THE GUARDIAN
131 SILAS MBISE WAPO MEDIA
132 SIMON RUGEGERA MKAI TV
133 SOMOE NG’ITU THE GUARDIAN LIMITED
134 STANSLAUS LAMBAT DAR24 MEDIA
135 STELLA T KESSY LAJIJI
136 SUZANA MAKORONGO MATUKIO BLOG
137 TAGATO J TAGATO TV3
138 THOBIAS ROMMY CELEB AFRICA TV
139 THOMAS JULIUS MSELEMU KANDANDA
140 TIMA SALEHE SIKILO SHIRIKA LA MAGAZETI YA SERIKALI ZANZIBAR
141 TUMAINI ABISSAY STEPHEN EATV & EA RADIO
142 URUGHU SALUMU BWIGANE TV
143 VENANT MTAKINGILWA GLOBAL PUBLISHERS
144 VICTORIA MUNGURE WAPO MEDIA
145 WALTER EZRAEL SIBUKA FM
146 WASTARA KHERI MSESE KISS FM TANZANIA
147 YUSUPH KATALAMBULA MIKASA TELE
148 ZAINA MOHAMMEDY AYOMA ONLINE TV
149 ZAMOYONI MBWALE TUZO ONLINE
150 ZUBERI HEMEDI MAKUNGE KITENGE TV