FEISAL HAKAMATIKI PASI ZA MABAO LIGI KUU YA NBC.

VITA ya pasi za mabao imezidi kushika kasi kutokana na namna wachezaji mbalimbali wanavyopambana kuhakikisha wanazidi kusaidia timu zao kupata alama za Ligi Kuu ya NBC.

Kiungo wa Azam Feisal Salum ndio kinara wa pasi za mwisho akiwa amecheza michezo 21 ya Ligi Kuu ya NBC, ndani ya dakika 1721 ameweza kutoa pasi za mabao nane.

Elie Mpanzu nae hayuko mbali amefanikiwa kucheza dakika 842 ndani ya michezo 17 ya Ligi Kuu ya NBC akitoa pasi za mabao saba mpaka sasa.

Allan Okello wa Young Africans ambaye aliingia dirisha dogo la usajili amecheza micheza 16 ambayo ni sawa na dakika 1128 amefanikiwa kutoa pasi za mabao saba.

Duke Abuya wa Young Africans anashika nafasi ya nne akiwa amecheza michezo 21 ya Ligi Kuu ya NBC sawa na dakika 1736 zilizomwezesha kutoa pasi za mabao tano.

Kwa upande wa Lamin Jarjou anaeichezea Singida Black Stars amecheza michezo 19 ikiwa sawa na dakika 1231 na kutoa pasi za mabao tano ndani ya Ligi Kuu ya NBC.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *