‘FEITOTO’ KINARA WA MABAO YA ‘UTOSI’ LIGI KUU YA NBC.

LICHA ya kujulikana zaidi kwa uwezo wao wa kucheza mpira wa chini na kutengeneza nafasi za kufunga, baadhi ya nyota wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026 wameonyesha ubora mkubwa wa kufunga mabao kwa kichwa.

Kiungo mshambuliaji wa Azam na raia wa Tanzania Feisal Salum (Feitoto), ndiye kinara wa orodha hiyo akiwa amefunga mabao manne 4 ya kichwa hadi sasa.

Feisal ameendelea kuwa silaha muhimu kwa Azam , akitumia vizuri mipira ya krosi na mipira ya adhabu kuisaidia timu yake kupata matokeo muhimu.

Nafasi ya pili inashikiliwa na mshambuliaji wa TRA United United, Mapaka Beatus aliyefunga mabao matatu 3 kwa kichwa.

Uwezo wake wa kuruka na kutumia nguvu za mwili umemfanya kuwa tishio kubwa kwa mabeki wa timu pinzani na kuisaidia TRA kupata matokeo mazuri hivi karibuni.

Mshambuliaji wa Tanzania Prisons Oscar Mwaijanga, anashika nafasi ya tatu akiendelea kuonyesha uwezo mkubwa wa kumalizia mashambulizi ndani ya eneo la hatari hasa kupitia mipira ya juu.

Nafasi ya nne inashikiliwa na Paul Peter wa JKT ambaye pia amefunga mabao matatu 3 ya kichwa.

Mchango wake umekuwa muhimu kwa JKT katika harakati za kutafuta matokeo mazuri msimu huu.

Hii inaonyesha kuwa mabao ya kichwa yameendelea kuwa sehemu muhimu ya ushambuliaji katika Ligi Kuu ya NBC msimu huu huku ‘Fei’ akiongoza orodha ya wachezaji waliotumia vyema mipira ya juu kuwatesa walinzi na makipa wa timu pinzani.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *