Geita Gold imeendelea kuonyesha ‘ubabe’ wake kwenye Ligi ya Championship ya NBC baada ya kutupia mabao 63 ikiwa ni idadi kubwa hadi sasa msimu wa 2025/2026.
Timu hiyo iliyopo katika mbio za kurejea Ligi Kuu ya NBC baada ya kushuka msimu wa 2023/2024 ikiwa ni takribani misimu miwili ikicheza Ligi ya Championship huku ikiongoza msimamo na alama 68.
Kagera Sugar iliyopo nafasi ya pili kwenye msimamo na Mbeya Kwanza iliyopo nafasi ya tatu nazo haziko nyuma ikiwa zimeweza kutikisa nyavu za wapinzani wake mara 52.
Polisi Tanzania ya mkoani Kilimanjaro ipo nafasi ya tatu kwa timu zenye mabao mengi ambapo imefunga mabao 47 yanayoiweka katika nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC.
Transit Camp haipo mbali ikiwa imetikisa nyavu za wapinzani wao mara 39 huku ikiwa nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi hiyo.
Kwa upande wa ‘wajeda’ wa Mbuni wenye maskani yake mkoani Arusha imefanikiwa kufunga mabao 37 ndani ya Ligi hiyo huku ikiwa nafasi ya sita katika msimamo.