FOUNTAIN GATE YASHINDWA ‘KUFURUKUTA’ KWA SINGIDA LIGI KUU YA NBC.

Ligi Kuu ya NBC mzunguko 24 imeendelea huku mchezo uliochezwa mkoani Manyara kati ya Fountain Gate na Singida Black Star ukishuhudia Fountain ikishindwa kutamba na kufungwa mabao 3-0.

Dakika ya 29 zilitosha kuipa uongozi Singida Black Star  kwa bao la kwanza kupitia mchezaji wake Jonathan Sowah aliyefunga bao lake la 7 tangu kujiunga na miamba hiyo ya Singida.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo Singida Black Star waliendelea kushambulia lango la Fountain Gate na mchezaji Frank Kwabena kuongeza bao la pili dakika ya 56 na dakika ya 71 mchezaji Emmanuel Kwame aliongeza bao la tatu kwa timu yake hivyo Singida Black Star kuongoza kwa mabao matatu na Fountain kumaliza bila bao mpaka mwisho wa mchezo.

Katika mchezo huo mchezaji kiungo wa Singida Black Star Keyeheh Emmanuel alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo huku Singida ikiwa nyuma ya Azam inayoshika nafasi ya tatu kwenye msimamo.

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *