FOUNTAIN GATE,SIMBA WATOSHANA NGUVU LIGI KUU NBC.

LIGI Kuu ya NBC imeendelea jana  mkoani Manyara ambapo  timu ya Fountain Gate Iliwakaribisha timu ya Simba katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa majira ya saa kumi alasiri.

Mchezo huo ulianza kwa kasi ambapo timu zote zilionekana kushambuliana kwa kasi kubwa  huku kila timu ikionyesha nia ya kuzitaka  alama tatu muhimu za mchezo huo jambo lilipolekea kwenda mapumziko wakiwa hawajafungana .

Kipindi cha pili kilianza ambapo dakika ya  57 mshambuliaji wa Simba, Leonel Ateba alifunga bao la  kwanza kwa timu yake   hivyo Simba kuwa mbele kwa  0-1.

Dakika ya 74 winga wa Simba Ladack Chasambi alijifunga goli  baada ya kupiga mpira  nyuma na golikipa wa Simba Moussa Camara  kushindwa kuumudu  ukaingia  nyavuni hivyo ubao kusomeka 1-1 mpaka mchezo huo unatamatika.

Simba ilifanikiwa kuvuna alama moja ugenini na kufikisha alama 44  wakiwa nafasi ya pili ya msimamo wakiwa wamefunga mabao 35 na kufungwa 6 katika mechi 17 ilizocheza mpaka sasa.

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *