GEITA ‘WAKALI’ WA KUTUPIA NBC CHAMPIONSHIP.

Geita Gold imeendelea kuonyesha ‘ubabe’ wake kwenye Ligi ya Championship ya NBC baada ya kutupia mabao 60 ikiwa ni idadi kubwa hadi sasa msimu wa 2025/2026.

Timu hiyo iliyopo katika mbio za kurejea Ligi Kuu ya NBC baada ya kushuka msimu wa 2023/2024 ikiwa ni takribani misimu miwili ikicheza Ligi ya Championship huku ikiongoza msimamo na alama 68.

Mbeya Kwanza nayo haiko nyuma ikiwa nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi hiyo imeweza kutikisa nyavu za wapinzani wake mara 51.

Kagera Sugar inayoshika nafasi ya pili kwenye msimamo imeweza kufunga mabao 49 ikiwa ni timu ya tatu kwa kufunga mabao mengi zaidi ndani ya Championship.

Polisi Tanzania ya mkoani Kilimanjaro ipo nafasi ya tatu kwa timu zenye mabao mengi ambapo imefunga mabao 47 yanayoiweka katika nafasi ya tatu ya msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC.

Transit Camp haipo mbali ikiwa imetikisa nyavu za wapinzani wao mara 38 huku ikiwa nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi hiyo.

Kwa upande wa ‘wajeda’ wa Mbuni wenye maskani yake mkoani Arusha imefanikiwa kufunga mabao 36 ndani ya Ligi hiyo huku ikiwa nafasi ya sita katika msimamo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *