LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Machi 8 kwa mchezo mmoja Kati ya Namungo na Yanga saa 12:00 jioni kwenye uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi.
Ikiwa Yanga itapata matokeo ya Sare au Ushindi itarejea moja kwa moja kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC nafasi ambayo inashikiliwa na Azam kwa sasa iliyopata sare kwenye mchezo wake wa mwisho dhidi ya Coastal Union ya Tanga.
Ushindi katika mchezo huu unaweza kuipeleka timu ya Namungo hadi nafasi ya nne kwenye msimamo kwani itafikisha alama 27 na kuizidi Coastal Union katika tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.