JKT Tanzania imefanikiwa kubakia Ligi Kuu ya NBC baada ya hii Leo kutoka suluhu na Tabora United kwenye mchezo wa pili wa mtoano hivyo JKT Tanzania kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-0.
Mchezo wa kwanza wa mtoano uliochezwa kwenye uwanja wa Ali hassan Mwinyi mkoani Tabora ulishuhudia wenyeji Tabora United wakikubali kichapo cha mabao 4-0 dhidi ya wageni wao JKT Tanzania.
Sasa Tabora United itakwenda kujaribu bahati yao ya kusalia Ligi Kuu ya NBC kwa kuwavaa Biashara United iliyokuwa ikishiriki Ligi ya NBC Championship, mchezo wa kwanza utachezwa Juni 12 mkoani Mara huku mchezo wa pili utachezwa Juni 16.
Mshindi wa jumla kwenye michezo hiyo miwili atashiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 na atakayepoteza atashiriki Ligi ya NBC ya Championship.