Jumla ya mabao 35 ya penati yamefungwa kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/2024 huku Said Ntibazonkiza akiibuka kinara kwa kufunga mabao Mengi (7).
Ntibazonkiza alifunga mabao hayo kwenye michezo dhidi ya Prisons, Kagera Sugar, KMC, Mashujaa, Singida FG, Geita Gold na JKT Tanzania.
Stephane Ki Aziz wa Young Africans anafuatia akifunga mabao matatu, Derick mukombozi wa Namungo FC akifunga mabao mawili sambamba na Lucas Kikoti wa Coastal Union huku waliosia wakifunga bao moja.