Kagera Sugar inashuka Dimbani hii leo Novemba 22 kuwakabili Polisi Tanzania kwenye muendelezo wa Ligi ya Championship ya NBC 2025/2026 mchezo utakao chezwa kwenye uwanja wa Kaitaba kuanzia saa 10:00 alasiri.
Kagera Sugar inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 13 sawa na Geita Gold inayoshika nafasi ya kwanza wakitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.
Kwa upande wa Polisi Tanzania ina jumla ya Alama 10 baaada ya michezo mitano ya Ligi ya Championship ya NBC ikishinda michezo mitatu, kufungwa mmoja na kutoka sare mchezo mmoja.
UShindi kwenye mchezo wa leo unaweza kuwapeleka ‘Wana Nkurukumbi’ Kagera Sugar kwenye kilele cha Ligi ya Championship ya NBC ikiwa mpinzani wake wa Karibu Geita Gold akipata matokeo mengine tofauti na ushindi.
Mkoani Tanga African Sports itaikaribisha Geita Gold kinara wa Ligi ya Championship ya NBC kwenye uwanja wa Mkwakwani mchezo utakaoanza saa 10:00 alasiri, Mchezo huu utarushwa Mubashara ‘Live’ kupitia FIFA+.