YOUNG AFRICANS YASHIKILIA ‘USUKANI’ LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC inazidi kushika kasi Iikielekea ukingoni huku timu ya Young Africans ikiendelea ilipoishia baada ya kuichapa Namungo 3-0 kwenye uwanja wa KMC Complex mkoani Dar es Salaam.

Ilimchukua dakika 27 kiungo wa Young Africans Aziz Ki kufungua ukurasa wa mabao na dakika nne baadae mshambuliaji wa timu hiyo raia wa Zimbabwe Prince Dube aliipatia timu yake bao la pili hivyo kwenda mapumziko ikiongoza 2-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi timu ya Namungo ikionekana kusaka namna ya kupata bao ambapo juhudi zao hazikuzaa matunda na dakika ya 74 mchezaji wa Young Africans Maxi Nzegeli aliipatia timu yake bao la tatu na mpaka dakika 90 zinatimia ubao wa matokeo ulikuwa unasoma 3-0.

Matokeo hayo yanaifanya Young Africans kufikisha alama 73 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu ya NBC huku timu hiyo ikisaliwa na michezo mitatu kuhitimisha Ligi hiyo.

Mchezaji wa Young Africans Maxi Nzegeli alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo kutokana na kiwango kizuri alichoonyesha katika mchezo huo akifunga bao na kutoa pasi ya bao la Stephane Aziz Ki.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *