KARIAKOO DABI KUPIGWA MEJA JENERALI ISAMUHYO.

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) inatangaza mabadiliko ya uwanja wa mchezo namba 169 wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026, kati ya klabu ya Simba na klabu ya Young Africans, maarufu kama ‘Kariakoo Derby’.

Mchezo huo ambao hapo awali ulipangwa kufanyika kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, sasa utachezwa kwenye uwanja wa Mej. Jenerali Isamuhyo mkoani Dar es Salaam Mei 3, 2026 kuanzia saa 12:00 jioni.

Sababu ya mabadiliko hayo ni uwanja wa Benjamin Mkapa kuwa kwenye matengenezo.

Klabu za Simba na Yanga pamoja na wadau wengine wa Ligi Kuu ya NBC wamepatiwa taarifa zote kuhusiana na mabadiliko ya uwanja wa mchezo huo na maandalizi yake yanaanza mara moja ili kuhakikisha unafanyika katika kiwango cha juu kinachoendana na hadhi ya michezo mikubwa ya Ligi ya sita kwa ubora barani Afrika.

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania inawatakia maandalizi mema wadau wote wa mchezo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *