YANGA, SIMBA ZAENDELEZA REKODI LIGI KUU YA NBC.

 

TIMU za Yanga na Simba zinashikilia rekodi za kipekee hadi hivi sasa kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu 2023/2024 zinapocheza viwanja vya nyumbani na ugenini kwa timu hizi.

Yanga ndio timu pekee ambayo haijapoteza mchezo wowote wa nyumbani kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu katika michezo 10 ya nyumbani Kati ya 20 iliyocheza mpaka sasa.

Simba inashikilia rekodi ya kutopoteza mchezo wowote wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu 2023/24 kwenye uwanja wa ugenini kwenye michezo 9 iliyocheza ugenini Kati ya 19.

Timu zote mbili Simba na Yanga zimepoteza michezo miwili kila mmoja ambapo Yanga ilipoteza dhidi ya Ihefu kwa mabao 2-1 Highland Estates mkoani Mbeya na 2-1 pia dhidi ya Azam FC kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa huku Simba ikipoteza dhidi ya Yanga 5-1 uwanja wa Benjamin Mkapa na 2-1 dhidi ya Tanzania Prisons mkoani Morogoro.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *