TABORA UTD, FOUNTAIN GATE ZATAKATA NYUMBANI LIGI KUU YA NBC.

 

MICHEZO miwili ya Ligi Kuu ya NBC imechezwa Septemba 11 katika mikoa ya Tabora na Manyara na kushuhudia timu mwenyeji wa mikoa hiyo Tabora UTD na Fountain Gate zikitakata.

Mchezo wa mapema saa 8:00 mchana Tabora UTD iliialika Kagera Sugar kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora na kumalizika kwa Tabora kushinda kwa bao 1 likifungwa kwa mkwaju wa penati na Asiegbu Shedrack.

Saa 10:00 jioni katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa Mkoani Manyara Fountain Gate ikaibamiza Kengold kwa mabao 2-1.

Kengold ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Joshua Ibrahim dakika ya 8 huku bao la kusawazisha la Fountain Gate likifungwa na Kassim Abdallah dakika ya 45, Selemani Mwalimu akafunga ukarasa wa mabao kwenye mchezo huo akifunga bao la pili na la ushindi kwa Fountain Gate.

Kwa matokeo hayo timu ya Tabora United imekwea mpaka nafasi ya nne baada ya kufikisha alama sita huku Fountain ikipanda hadi nafasi ya tatu ikiwa na alama sita zikitofautiana kwa mabao ya kufunga

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *