LADHA ZA LIGI KUU YA NBC KUREJEA APRIL MOSI

LIGI Kuu ya NBC inatarajia kurejea mapema mwezi ujao baada ya mapumziko ya takribani wiki mbili  kupisha michezo ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2026.

Kurejea kwa Ligi Kuu ya NBC ni mwanzo wa mzunguko wa  24  huku ikibaki mizunguko takribani sita ligi hiyo kutamatika.

April mosi Tabora United  itawakaribisha ‘watoto wa Jangwani’ Young Africans kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi  mkoani Tabora mchezo utakaochezwa majira ya saa kumi alasiri.

April mbili itapigwa michezo mitatu Pamba Jiji itaikaribisha Namungo majira ya saa 8:00 mchana katika  uwanja wa CCM Kirumba huku KMC ikiwaalika Tanzania Prisons kwenye uwanja wa KMC Complex mkoani Dar es Salaam majira ya saa 10:15 na mchezo wa mwisho utapigwa Tanzanite Kwaraa kati ya Fountain Gate itakayoikaribisha Singida Black Stars saa 10:15 alasiri.

April tatu itaanzia katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo JKT Tanzania ikiwakaribisha Dodoma Jiji, Ken Gold ikiwaalika Azam katika uwanja wa Sokoine michezo yote ikichezwa saa 10:00 alasiri huku Kagera Sugar ikiwaalika Coastal Union katika uwanja wa Kaitaba majira ya saa 1:00 usiku.

Mchezo wa Simba na Mashujaa utachezwa Mei mbili kutokana na timu ya Simba kukabiliwa na michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika ambayo kwa sasa ipo katika batua ya robo fainali.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *