LIGI KUU NBC KUWAKA VIWANJA VITATU LEO.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo kwa michezo mitatu itakayochezwa kwenye viwanja vitatu tofauti, miwili ikipigwa jijini Dar es salaam na mwingine mkoani Lindi.

Mchezo wa kwanza utazikutanisha timu za KMC dhidi ya Fountain Gate kwenye uwanja wa KMC Complex uliopo Dar es Salaam  saa 10:00 alasiri.

Fountain Gate inashika nafasi ya nane katika msimamo wa Ligi Kuu  ya NBC ikiwa na alama 24 huku KMC ikiwa nafasi ya11 na alama 24.

Mchezo mwingine utachezwa  saa 1:00 usiku kati ya Namungo ya mkoani Lindi na Singida Black Stars ya Singida kwenye uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi.

Namungo ipo nafasi ya 12 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 23 na Singida BS ikishika nafasi ya nne baada ya kukusanya alama 41.

Mchezo wa tatu utachezwa saa 3:00 usiku kati ya Azam iliyotoka sare na Namungo kwenye mchezo uliopita dhidi ya Tanzania Prisons itakayokuwa ugenini kwenye uwanja wa Azam  Complex, Dar es Salaam.

Azam iliyoshindwa kupata ushindi kwenye michezo mitatu ya Ligi Kuu ya NBC mfululizo itajiuliza dhidi ya Prisons iliyopoteza mchezo wake uliopita ugenini dhidi ya Fountain Gate huku ‘Maafande’ hao wakiwa juu ya mstari wa kushuka daraja kwa nafasi moja pekee.

One comment

  1. Pongezi kwa majukumu mazito na mnayafanyia kazi
    ombi langu ni juu ya uchapishaji wa taarifa unachelewa kidogo

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *