MICHEZO YA JKT LIGI KUU YA NBC YAAHIRISHWA.

MCHEZO wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Simba dhidi ya JKT Tanzania uliopaswa kuchezwa kesho Oktoba 29 umeahirishwa kutokana na timu ya JKT Tanzania kupata ajali ya basi eneo la Mbweni Dar es Salaam wakitokea Dodoma jana.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Afisa Habari na Mawasiliano wa Bodi ya Ligi Tanzaia (TPLB), Karim Boimanda amesema kuwa baada ya kupokea taarifa ya ajali hiyo Bodi ya Ligi ilifanya mawasiliano na timu ya JKT na pia ilipokea taarifa ya Daktari aliyewapokea majeruhi na iliwasiliana na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF kupitia kamati ya Tiba ya Shirikisho hilo ambapo Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Manfred Limbanga alikwenda hospitali kuwaona majeruhi ambapo alikuta wanaendelea vizuri.

Sambamba na hilo Boimanda alisema kuwa mchezo wa Ligi Kuu kati ya Namungo dhidhi ya JKT uliopaswa kuchezwa November 4 katika Uwanja wa Majaliwa Ruangwa Lindi umeahirishwa na michezo yote miwili itapangiwa tarehe nyingine.

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania inawatakia kheri majeruhi wote wa ajali hiyo na kuwaombea wapone haraka waweze kurejea katika majukumu yao ya kila siku.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *