LIGI KUU YA NBC KUREJEA LEO.

LIGI Kuu ya NBC inarejea leo baada ya mapumziko ya michezo ya kalenda ya Fifa ambapo timu ya Singida Black Stars itaikaribisha timu ya Azam katika uwanja wa Airtel mkoani Singida saa 10:00 alasiri.

Mchezo huo ni muhimu kwa timu zote kwani zinatafuta alama tatu muhimu ili kujiweka katika nafasi nzuri ya mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC.

Wachezaji wa timu ya Singida Black Stars.

Singida Black Stars iko nafasi ya sita katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 15 ikishinda michezo saba sare nne na kufungwa michezo minne ikikusanya alama 25.

 Wachezaji wa Azam

Kwa upande wa Azam ipo nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 15 kushinda michezo saba na sare nane huku ikiwa imekusanya alama 29.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *