LIGI Kuu ya NBC imeendelea leo kwa michezo miwili, JKT Tanzania wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani CCM Kambarage mkoani Shinyanga wametoka sare ya bao moja na Kagera Sugar.
Bao la JKT lilifungwa na Danny Lyanga Dakika ya 90+6 kwa mkwaju wa penati huku bao la Kagera Sugar likifungwa na Gasper Mwaipasi dakika ya 90+8.
Ukiwa mchezo wao wa kwanza katika uwanja wa Nyumbani Mkwakwani, Coastal Union imetoka suluhu dhidi ya Tabora United.
Ligi Kuu ya NBC itaendelea tena kesho Septemba 30 kwa michezo miwili, Geita Gold watawaalika KMC huku Namungo wakicheza na Mashujaa.