TMA KINARA NBC CHAMPIONSHIP.

TIMU ya TMA FC ya Arusha imeendeleza mwanzo mzuri wa Ligi ya Championship ya NBC kwa ushindi wa mabao 2-1 ugenini dhidi ya Pan African ya Dar .

TMA imecheza mchezo wa nne mfululizo bila kupoteza ikifikisha alama nane na kuongoza msimamo wa Ligi ya Championship huku ikiwa mojawapo ya timu zilizopanda daraja msimu huu.

Mkoani Mara timu ya Biashara United imeshindwa kutumia vizuri uwanja wa nyumbani na kulazimishwa sare ya bao moja dhidi ya Pamba ya Mwanza.

Ligi hiyo itaendelea tena Septemba 30 kwa michezo mitatu kati ya Stand United na Copco saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa Kambarage, Shinyanga huku Transit Camp ikicheza na Polisi Tanzania kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro na Green Warriors dhidi ya FGA Talents kwenye uwanja wa Uhuru, Dar michezo itakayochezwa saa 10:00 alasiri.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *