LIGI YA CHAMPIONSHIP YA NBC KUANZA LEO.

MSIMU mpya wa Ligi ya Championship ya NBC unatarajiwa kuanza kutimua vumbi leo kwa michezo miwili itakayopigwa kwenye mikoa miwili tofauti.

Michezo yote inatarajiwa kuanza saa 10:00 alasiri, Mbeya City itakuwa mwenyeji wa Bigman FC kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya huku Mtibwa Sugar iliyoshuka daraja kutoka Ligi Kuu ya NBC itakuwa mwenyeji wa Green Warriors kwenye uwanja wa Manungu Complex, Morogoro.

Ligi hiyo itaendelea tena Septemba 21, kwa michezo mitatu itakayopigwa kwenye mikoa mitatu tofauti.

Songea United itaialika Mbeya Kwanza kwenye uwanja wa MajiMaji, Ruvuma huku Cosmopolitan ikiialika African Sports kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro na mchezo wa mwisho utapigwa kwenye uwanja wa Nyankumbu, Geita kati ya Geita Gold na TMA ya Arusha.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *