LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa ya Tabora na Kagera.
Mkoani Tabora, Tabora UTD ilikuwa mwenyeji wa Fountain Gate katika uwanja wa Ali hassan Mwinyi saa 10:00 alasiri na kushuhudia Tabora ikikubali kichapo cha mabao 1-3.
Kwa matokeo hayo Fountain Gate imefikisha alama 10 kwenye michezo mitano ambazo zinaipandisha hadi nafasi ya pili kwenye msimamo nyuma ya Singida Black Stars.
Mkoani Kagera, Kagera Sugar ikaiadhibu Kengold kwa mabao 2-0 mabao yaliyofungwa na Peter Lwasa dakika ya 1 na 65, huu ni ushindi wa kwanza msimu huu kwa Kagera Sugar.
Kengold inaendelea kusota nafasi ya mwisho katika msimamo ikiwa ndiyo timu pekee ndani ya Ligi Kuu ya NBC msimu huu ambayo haijapata alama yoyote.