MABINGWA WAWILI ‘KUKIWASHA’ LEO AZAM COMPLEX.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Agosti 29 kwa mchezo mmoja kati ya Yanga na JKT Tanzania kwenye uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam kuanzia saa 1:00 usiku.

Mchezo huu unaikutanisha Yanga iliyokuwa bingwa wa Ligi Kuu NBC msimu uliopita na JKT iliyokuwa bingwa wa Ligi ya Championship msimu uliopita.

Timu hizo zinacheza mchezo wa pili wa ligi msimu huu kila moja ikiwa haijafungwa bao lolote na zote zikifanikiwa kushinda michezo yao ya ufunguzi.

Yanga ndiye kinara wa ushindi anapokutana na JKT akishinda michezo mitano kati ya sita waliyokutana huku wakitoka sare katika mchezo mmoja.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *