TIMU ya Yanga imeshinda mchezo wa pili mfululizo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kufunga mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania.
Mabao ya Stephane Ki Aziz, Kenedy Musonda, Kouasi Yao, na Maxi Nzengeli aliyefunga mawili yametosha kuiweka Yanga nafasi ya kwanza msimu huu ikiwa bingwa mtetezi kwa kufikisha alama sita.
Mpaka sasa timu ya Yanga ndio kinara wa kufunga mabao (10) huku ikiwa haijafungwa bao lolote sawa na timu za Mashujaa, Geita Gold na Singida Big Stars.
Yanga imeendeleza ubabe kwa JKT kwa kushinda michezo sita kwenye michezo saba iliyopita wakitoka sare mchezo mmoja .
Ligi Kuu ya NBC itaendelea tena Agosti 31, kwa mchezo mmoja wa kukamilisha mzunguko wa pili kati ya Singida Big Stars na Tabora United kwenye uwanja wa Liti, Singida.