MTIBWA HASHIKIKI NBC CHAMPIONSHIP.

 

LIGI ya NBC Championship Mzunguko wa 16 ulianza jana Januari 24 kwa michezo mitatu kuchezwa kwenye mikoa mitatu tofauti.

Mkoani Mtwara, Mbeya kwanza iliibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya Songea United, ushindi ulioipandisha Mbeya kwanza hadi nafasi ya nne kwenye msimamo ikifikisha alama 30.

African Sports ya Tanga iliifunga Cosmopolitan ya Dar es salaam kwa mabao 2-1 mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa TFF Center mkoani Tanga.

Mtibwa Sugar ikiwa ugenini Mkoani Pwani ikaifunga Green Warriors kwa mabao mawili kwa moja mchezo ambao ulichezwa katika uwanja wa Mabatini.

Ushindi huo wa Mtibwa unaifanya kufikisha alama 41 na kuendelea kujichimbia kileleni mwa msimamo wa Ligi ya Champiomship ya NBC kwa tofauti ya alama saba na timu inayomfuatia Mbeya City.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *