LIGI ya NBC Championship imeanza rasmi kwa michezo miwili ya ufunguzi ikizihusisha timu za Mtibwa na Green Warriors, Mbeya City na Big Man FC.
Mtibwa imeanza Ligi ya NBC Championship kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Green Warriors mabao yote yakifungwa na Raizin Hafidh, mchezo uliochezwa saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa manungu, Morogoro.
Mbeya City ikiwa nyumbani ikalazimishwa sare ya mabao 2 na Big Man FC mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine saa 10:00 alasiri.
Mchezaji wa Mbeya City Malick Joseph anaingia kwenye kumbukumbu za Ligi ya NBC Championship msimu huu kuwa mchezaji aliyefunga bao la kwanza la Ligi hiyo.
Kifaru sasa anatamba championship watatoboa kweli?