‘WAZEE’ WA ‘MAKOMBORA’ YA LIGI KUU YA NBC.

Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026 imeendelea kushuhudia mabao ya kuvutia kutoka nje ya eneo la hatari, huku baadhi ya nyota wakionyesha uwezo mkubwa wa kupiga mashuti sahihi yanayowapa mashabiki burudani ya kipekee.

Kinara wa orodha hiyo ni mshambuliaji wa Azam Idd Seleman ambaye hadi sasa ameweka kambani mabao matano akifunga kutoka nje ya eneo la 18 ambapo wezo wake wa kupiga mashuti ya kushtukiza umekuwa silaha muhimu kwa Azam katika harakati za kutafuta mafanikio msimu huu.

Nafasi ya pili inashikiliwa na kiungo mshambuliaji wa Simba Clatous Chama aliyefunga mabao manne kutoka nje ya eneo la 18.

Chama ameendelea kuthibitisha ubora wake wa muda mrefu kwa kutengeneza nafasi na kufunga mabao muhimu katika nyakati ngumu za mchezo zinazowafanya Simba kuendelea kusalia kwenye mbio za ubingwa.

Katika nafasi ya tatu ni nyota wa Mtibwa Sugar Ismail Mhesa, mwenye mabao matatu ya nje ya boksi likiwemo lile alilofunga kwa mpira wa kona ulioingia moja kwa moja dhidi ya Young Africans.

Beki wa Singida Black Stars, Ibrahim Imoro ambaye licha ya kucheza nafasi ya ulinzi amekuwa tishio kubwa kupitia mashuti yake ya mbali na mipira ya adhabu nae amefunga matatu sawa na Mhesa.

Kadri msimu unavyoelekea ukingoni mashabiki wataendelea kutarajia kuona mabao mengi zaidi ya kuvutia kutoka kwa nyota hawa wenye uwezo wa kubadili matokeo ya mchezo kwa shuti moja tu lililo sahihi.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *