TMA, POLISI ZATAKATA NBC CHAMPIONSHIP LEO.

 

LIGI ya NBC Championship imeendelea leo Januari 6, kwa michezo minne kupigwa kwenye mikoa mitatu tofauti.

Mkoani Pwani michezo miwili ilipigwa kwenye uwanja wa Mabatini huku mapema saa 8:00 mchana Pan African waliwaalika Copco na mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao moja, saa 10:00 alasiri Green Warriors wakawaalika Mbeya City na kumalizika kwa suluhu.

Polisi Tanzania wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani ushirika mkoani Kilimanjaro saa 8:00 mchana wakawakaribisha Mbeya Kwanza na kuibuka na ushindi wa bao moja.

Mkoani Shinyanga saa 10:00 alasiri Stand United ikawakaribisha TMA kwenye uwanja wa Mwadui Complex na Stand United kukubali kichapo cha mabao 1-6.

Kwa matokeo hayo TMA wanapanda hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wakiwa na jumla ya alama 33 baada ya michezo 16.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *