Ligi ya NBC Championship itaendelea leo Septemba 15 kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa ya Kilimanjaro na Mwanza.
Polisi Tanzania watakuwa wenyeji wa Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Ushirika, Kilimanjaro saa 8:00 mchana huku mchezo huo ukitarajiwa kutangazwa Mbashara kupitia chaneli ya TV3.
Baaada ya kupata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Cosmopolitan kwenye mchezo wa kwanza Pamba watakuwa uwanja wa Nyamagana, Mwanza saa 10 alasiri kuwaalika Pan Africans waliopata ushindi wa mabao 3-2 katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya Copco ugenini.
Jumla ya mabao 25 yamefungwa mpaka sasa kwenye ligi ya NBC Championship katika michezo minane iliyochezwa mzunguko wa kwanza.