NI VITA YA KUBAKI NA KUPANDA FIRST LEAGUE LEO.

Michezo ya mtoano (PlayOff) ya kubaki na kupanda First League inachezwa leo Mei 8 ikikutanisha timu mbili kutoka First League ambazo ni Tunduru Korosho ya Ruvuma na Copco ya Mwanza pamoja na timu mbili kutoka kwenye Fainali za mabingwa wa mikoa ambazo ni Cargo ya Dar es Salaam na Kajuna ya Kigoma.

Mechi ya kwanza itakutanisha timu ya Cargo dhidi ya Tunduru Korosho saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa TFF Center Kigamboni uliopo Dar.

Mechi ya pili itakutanisha timu ya Kajuna dhidi ya Copco kwenye uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma huku mchezo huo ukitarajiwa kupigwa saa 10:00 alasiri.

Ikumbukwe timu mbili kutoka First league ni zile zilizopoteza michezo ya Mtoano wa kushuka daraja (Relegation Playoffs) na kupata nafasi ya kupambania kubakia kwenye Ligi hiyo kwa msimu ujao.

Timu mbili kutoka Fainali za mabingwa wa mikoa ni zile zilizotolewa kwenye Nusu Fainali na kushika nafasi ya tatu na ya nne kwenye fainali hizo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *